Posts

Showing posts from August 25, 2023

COSTECH YAFADHILI MIRADI YA UTAFITI KUHUSU SOMO LA HISABATI

Image
Na Janeth Raphael - MichuziTv - Dodoma. TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imefadhili miradi miwili wenye thamani ya Sh.milioni 120 kwa kila mradi kwa lengo la kufanya utafiti katika somo la hisabati kutokana na matokeo mabaya ya somo hilo katika mtihani wa darasa la saba na kidato cha nne. Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt.Amos Nungu Akizungumza leo Agosti 25,2023 na waandishi wa habari jijini Dodoma Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu amesema  imeidhinisha miradi miwili kwa thamani ya Sh.milioni 120 kila mradi na utekelezaji wa mradi unahusisha watafiti kutoka vyuo mbalimbali hapa nchini. Amefafanua mradi utafanyika katika kipindi cha miaka miwili na hatua iliyopo sasa ni kusaini mikataba. "Somo la hisabati bado ni changamoto kwani matokeo yake yamekuwa mabaya kwa kidato cha nne na darasa la saba. " Hivyo kwa kuondoa tatizo hilo  Tume tumeidhinisha miradi miwili ambayo kila mmoja thamani yake ni Sh.milioni 120,"amesema na kuongeza miradi m...

RAIS SAMIA AZUNGUMZA KWENYE MKUTANO WA 15 WA BRICS UNAOFANYIKA JOHANNESBURG NCHINI AFRIKA KUSINI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Iran Mhe. Dkt. Seyyed Ebrahim Raisi kabla ya kuanza mazungumzo kando ya mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Iran Mhe. Dkt. Seyyed Ebrahim Raisi kabla ya kuanza mazungumzo kando ya mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisoma hotuba yake kwenye Mkutano wa 15 wa BRICS unaofanyika Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini

TRA YAZINDUA KAMPENI KUELEZEA UMUHIMU RISITI ZA MASHINE ZA EFD

Image
Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kikodi Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Husna Nyange amesema kodi sahihi inatokana na kumbukumbu sahihi za kikodi hivyo amewahimiza wafanyabiashara kutoa risiti kila wanapofanya mauzo. Pia na wanunuzi kudai risiti sahihi za EFD kila wanaponunua bidhaa au kupata huduma lengo likiwa kila mmoja kwa nafasi yake anatunza kumbukumbu zake. Nyange ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa mabango ya uhamasishaji kuhusu matumizi sahihi ya EFD. Hivyo pamoja na mambo mengine ameelezea umuhimu wa wafanyabiashara kuwa na kumbukumbu sahihi za kikodi hivyo lakini wanunuzi nao ni vema wakajenga utamaduni wa kudai risiti kutoka kwa wafanyabiashara. Kwa upande wake Meneja Msaidizi wa Huduma kwa Mlipakodi Mkoa wa kikodi Kinondoni Emanuel Lucian Dafay amesema kampeni hiyo ya EFD ni endelevu na kwa mkoa wa Kinondoni walianza kwa kutuma ujumbe mfupi (sms) kwa wafanyabiashara kupitia simu zao za mkononi. Amefafanu leng...

MENEJIMENTI YA TANESCO YARIDHISHWA NA UJENZI WA MRADI WA BWAWA LA KUFUA UMEME WA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Image
  Na Neema Mbuja, Rufiji Timu ya Menejimenti ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) imetembelea mradi wa Bwawa la Julius Nyerere JNHPP huku ikieleza madhumuni ya ziara hiyo ikiwemo kufanya tathimini ya mwenendo wa ujenzi wa mradi unaokaribia asilimia 91 ifikapo Agosti mwishoni. Lengo jingine la ziara hiyo ni kuangalia mwenendo wa ujenzi wa mradi na tathimini ya hali ya mvua za vuli zinazotarajiwa kunyesha kati ya Oktoba hadi Disemba kama ilivyotangazwa na Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa Tanzania (TMA).Timu hiyo imeongozwa na Mkurugenzi mkuu wa Tanesco Maharage Chande. Akizungumza na waandishi wa habari, Chande amesema maendeleo ni mazuri hadi Julai tulifikia asilimia 90 na tunatarajia mwishoni mwa Agosti tutafikia asilimia 91 huku akiwapongeza wahandisi na wafanyakazi wa shirika hilo wanaosimamia mradi huo.   Amesema ukamilikaji wa mradi huu utatuwezesha kushinda mashindano haya kwa kuwa na umeme wa uhakika utakaokidhi mahitaji ya uchumi. Amesema timu ya menejim...

MTENDAJI MKUU TARURA AZUNGUMZIA UTEKELEZAJI, MAJUKUMU NA MWELEKEO WA WAKALA HIYO MWAKA WA FEDHA 2023/24

Image
  YALIYOJIRI LEO WAKATI MTENDAJI MKUU WA WAKALA YA BARABARA ZA VIJIJINI NA MIJINI (TARURA), MHANDISI VICTOR SEFF AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU WA WAKALA HIYO NA MWELEKEO WAKE KATIKA MWAKA WA FEDHA 2023/24 Mtendaji Mkuu wa TARURA, Eng. Victor Seff akiongea na wanahabari #Jukumu kubwa la TARURA ni kusimamia ujenzi, ukarabati na matengenezo ya mtandao wa barabara za Wilaya. Serikali ya Awamu ya Sita imeiongezea TARURA bajeti yake mara tatu zaidi ikiwa ni kuendeleza juhudi za Awamu zilizopita za kuboresha barabara za vijini. #Kwa sasa TARURA ipo kwenye utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Pili toka kuanzishwa kwake mwaka 2017 ikiwa na lengo kuwa, ifikapo mwaka 2025 angalau asilimia 85 ya barabara za Wilaya ziwe zinapitika kwa misimu yote. #Lengo hilo linaakisi kaulimbiu ya TARURA Mpango Mkakati wa Pili inayosema "TARURA tunakufungulia barabara kufika kusikofikika." #Mtandao wa barabara za Wilaya chini ya TARURA una jumla ya kilomita 144,429...

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LATAKIWA KUKUSANYA MADENI

Image
Na Munir Shemweta, WANMM Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii imelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuhakikisha linatilia mkazo ukusanyaji madeni ya wapangaji katika nyumba zake. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii Timotheo Mnzava akizungumza wakati Kamati yake ikipokea taarifa ya Shirika la Nyumba la Taifa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Timetheo Mnzava amesema, pamoja na shirika hilo kujitahidi katika ukusanyaji malimbikizo ya kodi za wapangaji wake lakini bado linatakiwa kuongeza kasi ya ukusanyaji madeni kutoka kwa wadaiwa. Akizungumza wakati wa Kikao cha kupokea taarifa ya utendaji kazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) jijini Dodoma tarehe 25 Agosti, 2023, Mhe. Mnzava amelitaka pia shirika hilo kuweka msisitizo zaidi katika kuzuia kuzalisha madeni badala ya kusubiri mpaka wapangaji kuwa na malimbikizo makubwa ya madeni. Aidha, Wajumbe wa Kamati hiyo ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Malisili na Utalii wametaka kuwepo mikakati madhubut...