Posts

Showing posts from March 5, 2025

Senyamule apigilia Msumari matumizi ya Nishati safi ya kupikia

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA   Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, ametoa wito kwa wananchi jijini Dodoma kutumia nishati safi ya kupikia ili kutunza mazingira na kulinda afya za wananchi kutokana na madhara ya matumizi ya nishati chafu ya kupikia.   Senyamule alisema hayo wakati wa mkutano wa hadhara katika Kata ya Nzuguni, baada ya kufanya ziara na kukagua miradi mbalimbali ya maendelea katika kata hiyo. ā€œRais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ameshaelekeza kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia nyumbani na katika sehemu za mikusanyiko, kwahiyo kama huwezi kununua mtungi wa gesi ni bora zaidi ukatumia nishati mbadala kama makaa ya mawe na kuni poa, kwasababu upatikanaji wake na gharama zake ni nafuu na rafiki kwa kila mmoja wetu kuweza kuzimudu, hilo litasaidia kuondokana na madhara ya kiafya yatokanayo na matumizi ya nishati chafu za kupikia, lakini pia itasaidia kutunza mazingira ya jiji letu na kuondokana na uhalibifu kama ukataji wa mkaaā€ alisema Seny...

Watumishi Zahanati Kitelela mambo shwari

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ametembelea na kukagua nyumba ya watumishi wa Zahanati ya Kitelela iliyopo Kata ya Nzuguni, Wilaya ya Dodoma na kuwataka watumishi kutoa huduma bora kwa wananchi. Nyumba hiyo ā€˜two in oneā€™ imegharimu kiasi cha shilingi 60,000,000 hadi kukamilika kwake, ikiwa na uwezo wa kukaliwa na familia mbili kwa pamoja. Baada ya kukagua nyumba hiyo alisema ā€œutekelezaji wa mradi huu ni muendelezo wa utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuhakikisha tunapunguza vifo vya mama na mtoto, hasa wakati wa kujifungua, dhamira ya mradi huu ni kuimarisha na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Mwanzoni huduma za afya zilikuwa zikitolewa lakini ikifika jioni huduma zinakuwa hazitolewi kutokana na wauguzi kuishi mbali na kituo cha afya. Lakini kwasasa muda wowote wananchi wa Kitelela na maeneo jirani wana uwezo wa kupata huduma muda wowote baada ya mradi huu wa nyumba za wauguzi kukamilikaā€.   N...