Posts

Showing posts from April 29, 2025

Wananchi washirikishwe katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA NAIBU Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago ametoa rai kuwa miradi yote ya maendeleo inayotekelezwa wananchi washirikishwe kikamilifu ili wawe sehemu ya miradi hiyo na kusema kuwa utaratibu huo utaifanya miradi kudumu kwa muda mrefu. Kauli hiyo aliitoa alipoongoza Kamati ya Fedha na Utawala timu namba tatu kutembelea na kukagua umaliziaji wa vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Msingi Nguji iliyopo Kata ya Ng’hong’onha, jijini Dodoma. Alisema kuwa halmashauri inatekeleza miradi mingi ya maendeleo. “Nitumie nafasi hii kuwasisitiza kuendelea kuwashirikisha wananchi wa eneo husika kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Wananchi wakishirikishwa wanakuwa wamiliki wa mradi husika. Wasiposhirikishwa wanajiona siyo sehemu ya mradi. Hata kama kuna mtu anataka kufanya uharibifu kwenye mradi, wananchi wanabaki wanamtazama kwa sababu hawajashirikishwa. Nitumie nafasi hii kutoa rai, kwenye miradi yetu tunapoitekeleza, tuwashirikishe wananchi ...

Shule mpya ya Kata, Sekondari Miyuji B yajengwa kisasa kutoa elimu bora

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA KAMATI ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imempongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nia yake njema ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora hasa za elimu baada ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo yenye zaidi ya shilingi 500,000,000 katika kata tatu za jiji hilo. Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago alipoongoza timu namba tatu ya Kamati ya Fedha na Utawala kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika kipindi cha robo ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2024/2025. Alisema kuwa kamati yake ilitembelea kata tatu za Ng’hong’ohna, Makole na Miyuji kukagua miradi ya maendeleo. “Leo tumekuwa na ziara nzuri ya kutembelea miradi mbalimbali katika kata tatu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kamati ya Fedha na Utawala tuligawana na kupeana majukumu ya kutembelea miradi ya maendeleo. Timu yangu tumekagua umaliziaji wa vyumba vitatu vya madarasa Shule ya Msingi Nguji, Kata ya Ng’hong’onha, uje...

Jengo jumuishi la kutolea huduma za Afya Makole lipo katika hatua nzuri ya ujenzi

Image
Na. Nancy Kivuyo, MAKOLE Mradi wa ujenzi wa jengo jumuishi la kutolea huduma za afya katika Kituo cha Afya Makole wenye zaidi ya shilingi bilioni moja lipo katika hatua nzuri ya utekelezaji wake. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makole, Dkt. Salma Gwassa alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Makole kwa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliyotembelea maendeleo ya mradi huo. Alisema kuwa kiasi cha shilingi 750,000,000 kimetolewa na serikali kuu na fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma shilingi 289,794,329 zimelipwa kwa mkandarasi kwaajili ya ujenzi huo. Alisema kuwa ujenzi upo katika hatua ya msingi na wanatarajia mradi utakapokamilika wananchi wa Kata ya Viwandani na Jiji la Dodoma kwa ujumla watapata matibabu hapo. “Mradi huu ukikamilika huduma za kliniki za kibingwa ‘speciality clinic’ zitapatikana, huduma za kiutawala zitaboreka na tutapanua wigo wa utoaji wa huduma kwa wagonjw...

Ujenzi wa Darasa Sekondari Anthony Mavunde kupunguza msongamano kwa wanafunzi

Image
Na. Nancy Kivuyo, HOMBOLO BWAWANI Mkuu wa Shule ya Sekondari Anthony Mavunde, Mwalimu Emmanuel Magumba amesema kuwa shule hiyo ilipokea kiasi cha shilingi 15,425,000 kwa ajili ya ujenzi wa darasa moja na ununuzi wa viti 50 na meza 50 kwa lengo la kuongeza miundombinu katika shule hiyo. Mwl. Magumba alisoma taarifa ya mradi huo mbele ya Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kusema kuwa pamoja na ujenzi unaoendelea anaiomba halmashauri iwaongezee fedha kwa ajili ya kumalizia darasa hilo. “Hatua tuliyofikia ni nzuri kwasababu umaliziaji darasa hili sio mkubwa kama unavyoanza ujenzi” alisema Mwl. Magumba. Aliongeza kuwa kukamilika kwa darasa hilo kutaleta chachu ya wanafunzi kusoma kwa bidii. “Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa ujenzi wa darasa hili ukikamilika naamini wanafunzi wetu watapata nafasi ya kusoma na wataongeza bidii katika masomo” aliongeza Mwl. Magumba. Nae, Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza, Emmanuel Mbega alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwajen...