Posts

Showing posts from August 29, 2024

Baraza la Madiwani la Jiji la Dodoma lapitisha Hesabu za Mwaka 2023/2024

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA Baraza la Madiwani la Jiji la Dodoma limefunga rasmi hesabu za mwaka wa fedha unaoishia tarehe 30 Juni 2024, baada ya kupokea, kujadili na kupitisha taarifa ya ufungaji wa hesabu za halmashauri. Kwa mujibu wa Mweka Hazina wa Halmashauri ya Jiji, CPA. David Rubibira alisema chanzo kikuu cha mapato ya halmashauri hiyo ni tozo, faini na ushuru mbalimbali. Mapato mengine yanatokana na michango ya afya, uwekezaji, pamoja na ruzuku kutoka Serikali Kuu, aliongeza. "Mapato na matumizi ya ndani ya halmashauri ni pamoja na mapato yenye tozo (kodi) ambayo ni kiasi cha shilingi bilioni 34.7, faini na tozo ni shilingi bilioni 2.6, Mapato mengineyo ni shilingi bilioni 6.6. Michango mengineyo ya afya ni shilingi bilioni 1.9, mapato yapatikanayo kwenye uwekezaji ni shilingi bilioni 5.5 na mapato toka serikali kuu ni shilingi bilioni 83.08 ambapo jumla ya mapato na matumizi yote ya ndani ya halmashauri ni shilingi bilioni 134.4" alisema CPA. Rubibira. Kwa upan...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapokea taarifa ya ufungaji hesabu mwaka 2023/2024

Image
Na. Jackline Patrick na Emmanuel Lucas, DODOMA Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwaajili ya kujadili taarifa ya ufungaji hesabu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2023/2024 umepokea, kujadili na kupitisha taarifa hiyo. Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira akichangia taarifa ya kufunga hesabu za halmashauri Mkutano huo ulifanyika leo tarehe 29 Agosti, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Wakati akichangia taarifa hiyo, Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikira alisema kuwa taarifa hiyo imeandaliwa vizuri. “Mstahiki Meya, kwanza tumeipokea taarifa na niipongeze timu ya wataalamu kwa kuandaa na kuwasilisha hii taarifa. Lakini la pili, Mstahiki Meya taarifa hii imetupa dira ya mwaka huu wa fedha kwenye yale mapungufu yaliyojionesha kwenye taarifa hii katika utekelezaji wa shughuli zetu za halmashauri, tukayafanyie kazi ili taarifa ya mwaka unaokuja basi haya mapungufu yaweze kupunguzwa kwa kiasi kikubwa. Taarifa hii itup...

Mstahiki Meya Jiji la Dodoma ahimiza Uwajibikaji

Image
Na. Francisca Mselemo, DODOMA Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri kupokea na kujadili taarifa ya kufunga hesabu hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2024. Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA David Rubibira Akiwasilisha taarifa hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA David Rubibira alisema kuwa taarifa hiyo inawasilishwa kwa mujibu wa sheria. “Mheshimiwa Mstahiki Meya, hesabu hizi sio ngeni. Naomba Baraza lako tukufu lifahamu kwamba ni zilezile ambazo huwa tunakutana na kuzijadili kila robo, za mapato na matumizi. Hii ni kwamba tu ni takwa la kisheria. Tunatakiwa tuziandae katika mpango wa uwasilishaji wa kimataifa. Umuhimu wa hizi hesabu ni kwamba ni takwa la kisheria, kwa maana tunapomaliza mwaka, kwa Halmashauri tunatakiwa kuwa na hesabu za mwaka husika, ambazo katika kipindi kisichozidi miezi mitatu baada ya mwaka kuisha, zinatakiw...

Madiwani Jiji la Dodoma wapitisha taarifa ya ufungaji hesabu za mwaka 2023/2024

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limepokea taarifa ya ufungaji wa hesabu kuishia tarehe 30 Juni, 2024 na kushauri kuwa changamoto zilizojitokeza katika mwaka ulioisha zitatuliwe ili zisijitokeze katika ufungaji hesabu ujao. Mwenyekiti wa Mkutano huo, Prof. Davis Mwamfupe akifungua mkutano Baada ya taarifa ya ufungaji wa hesabu kuishia tarehe 30/6/2024 kuwasilishwa kwenye mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya ufungaji wa hesabu iliyowasilishwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhasibu na Fedha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wajumbe waliipokea. Mwenyekiti wa Mkutano huo, Prof. Davis Mwamfupe aliwahoji wajumbe kama wanaipokea taarifa hiyo na kwa kauli moja waliipokea taarifa hiyo. Alisema kuwa taarifa hiyo imehusisha mapendekezo ya Kamati ya Fedha na Utawala kama walivyoshauri. Akiwasilisha taarifa ya ufungaji hesabu za halmashauri kuishia tarehe 30 Juni, 2024, Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu, CPA Da...