Vijana waalikwa kushiriki Kongamano S/M Mbwanga
Na. Mwandishi Wetu Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kujitokeza na kushiriki kongamano la vijana la Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025 lenye lengo la kutoa elimu kuhusiana na fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo nchini. Mwenyekiti wa Kamati ya Kongamano la Vijana katika mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025, Abeid Msangi Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kongamano la Vijana katika mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2025, Abeid Msangi akiongelea maandalizi ya kongamano hilo litakalofanyika katika Shule ya Msingi Mbwanga iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa kongamano hilo limeandaliwa kwa ajili ya vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Nichukue nafasi hii kuwahamasisha vijana wa Jiji la Dodoma kujitokeza kwa wingi katika kushiriki kongamano hilo. Kongamano hilo linalenga kuwajenga vijana kuwa wazalendo, kuifahamu historian a falsafa ya Mwenge wa Uhuru. Pia tutatoa elimu kwa vijana kuhusiana na umuhimu wa kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa aman...