Posts

Showing posts from August 7, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma atembelea Kijiji cha Mitambo, Nanenane

Image
  Mkuu wa Mkoa, Rosemary Senyamule Agosti 7, 2025 ametembelea Kijiji cha Mitambo (Mechanisation Village) kilichosheheni teknolojia mbalimbali za kilimo cha umwagiliaji kinachopatikana katika Maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi maarufu kama Nanenane Kitaifa 2025 Kanda ya Kati yanayoendelea kwenye viwanja vya Nzuguni jijini hapa. Vilevile, Senyamule akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri, wametembelea mabanda kadhaa yakiwemo; Tume ya Ushindani, Chuo cha Biashara na Elimu (CBE), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Madini (STAMICO), VETA, Wizara ya Maendeleo ya Jamii na TBA na kujionea mambo mbalimbali yanayofanywa na Taasisi hizo

Wafugaji wahamasishwa kutumia Mbegu bora za Malisho ili kuleta tija kwenye mifugo

Image
Na. Hellen Minja, DODOMA RS Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepiga hatua katika kuongeza upatikanaji wa mbegu bora za malisho ya kupandwa (majani) yanayoleta tija kwa wafugaji kutokana na kuifanya mifugo kuwa na uzito mkubwa unaoongeza thamani yake sokoni na kuthibitisha kaulimbiu ya 'Ufugaji ni utajiri'. Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, aliposhiriki Maonesho ya Gwaride (Paredi) la Wanyama lililofanyika kwenye viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma sanjari na Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2025 Kanda ya Kati. “Sasa hivi wafugaji wameanza kuelewa umuhimu wa kutumia majani ya kupandwa kwa ajili ya mifugo au malisho, hatua hii ni kubwa na tunaipongeza sana na sasa tumeona wizara imepanga kuendeleza upatikanaji wa mbegu bora. Yote haya yanafanywa ili wafugaji waweze kupata uwezeshaji” alisema Senyamule. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede alitoa wito kwa wafuga...

Elimu ya Lishe inapatikana Banda la Nanenane Jiji la Dodoma

Na. Mwanaidi Masudi, DODOMA Mjasiriamali kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Agnes Kinyaii, ametoa elimu ya kina kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa wananchi waliojitokeza kwenye maonesho ya Nanenane kitaifa yanayofanyika jijini Dodoma.   Akizungumza katika banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Kinyaii aliwasisitiza wananchi kuzingatia ulaji wa lishe bora kama utumiaji wa viazi vya ‘bitreat’ vinavyosaidia mambo makuu manne kuongeza damu, kukinga maradhi ya damu na afya ya mifupa ya meno.   Aliendelea kuelezea kuwa upo unga wa lishe uliotengenezwa katika utaratibu ambao unampatia mtu virutubisho zaidi ya kushiba. “Kwamba tumechanganya vitu vikuu vinne, tumeweka mahindi lishe na viazi lishe, mbegu nyeusi za maboga. Lakini pia tumeweka ‘Almond’ na ngano isiyo kobolewa. Kwahiyo, huu unga anatumia mtoto mdogo anayeanza kula mpaka mzee na ukila hauwezi kukuzidi nguvu kwasababu hatujazidisha wanga. Tumeweka vitu viwili vinavyotoa wanga yaani viazi na mahindi lishe ambayo y...