Posts

Showing posts from September 17, 2026

Habitat for Humanity yaunga mkono usafi Soko la Sabasaba

Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Shirika la Habitat for Humanity Tanzania limeunga mkono juhudi za kuimarisha usafi katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma kwa kutoa vifaa mbalimbali vitakavyotumika katika shughuli za usafi wa mazingira. Mratibu wa shirika hilo, Elnoth Lekaaya alisema kuwa wameweza kushirikiana na wadau wa maendeleo pamoja na Jiji la Dodoma katika kuhakikisha suala la usafi linafanyika kwa ufanisi katika maeneo ya jamii. Alisema kuw kupitia ushirikiano huo, shirika limechangia vifaa vya usafi vyenye thamani ya shilingi milioni moja, vikiwemo mifagio, reki, toroli na vifaa vingine mbalimbali. Lekaaya alisema kuwa msaada huo unalenga kuwawezesha wafanyabiashara na wadau wengine kushiriki kikamilifu katika kutunza mazingira ya soko, ili wananchi wanaofika kwa shughuli mbalimbali waweze kupata mazingira safi na salama. Aliongeza kuwa Habitat for Humanity Tanzania inatekeleza shughuli zake katika maeneo mbalimbali yanayolenga kuboresha maisha ya jamii, ikiwemo masuala...

RC Dodoma amtaka Mkandarasi kuongeza kasi ukarabati Soko la Majengo

Image
Na. Mohammed Ramadhani, MAJENGO Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amemtaka mkandarasi anayetekeleza ukarabati wa Soko la Majengo jijini Dodoma kuongeza kasi ya kazi ili kukamilisha mradi huo ndani ya muda wa nyongeza wa siku 60 uliotolewa. Senyamule alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa Soko la Majengo, akieleza kuwa soko hilo lina mchango mkubwa katika kutoa huduma na kukidhi mahitaji ya wananchi wa Jiji la Dodoma. Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa utekelezaji wa kazi unaelekea vizuri, lakini mkandarasi anapaswa kutumia kikamilifu muda wa nyongeza aliopewa ili kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika kwa wakati. Aidha, alishauri kuwa mkandarasi kuongeza muda wa utekelezaji wa kazi kwa kufanya kazi hadi nyakati za usiku kwa kutumia taa, akisema hatua hiyo itasaidia kuongeza kasi ya ujenzi na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati. Alisisitiza umuhimu wa kukamilisha kazi kabla ya kuanza k...

Usafi Soko la Sabasaba watakiwa kufanyika kila siku

Image
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Diwani wa Kata ya Viwandani, Swalihina Athuman amewataka viongozi na wafanyabiashara katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma kuimarisha usimamizi wa usafi wa mazingira, akisisitiza kuwa usafi wa soko hilo unapaswa kuwa jukumu la kila siku kutokana na umuhimu wake kwa shughuli za biashara na afya za wananchi. Athuman alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kuhusu hali ya usafi katika Soko la Sabasaba, akieleza kuwa soko hilo ni miongoni mwa masoko makubwa yanayohudumia wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma, hivyo linahitaji usimamizi madhubuti wa mazingira ili kuhakikisha shughuli za biashara zinafanyika katika mazingira salama. Diwani huyo alisema kuwa mazingira ya soko hilo yana mchango mkubwa katika ustawi wa wafanyabiashara na wateja, hivyo kila mmoja anapaswa kutambua wajibu wake katika kuhakikisha taka zinadhibitiwa na maeneo ya biashara yanakuwa safi wakati wote. “Tusipokuwa makini kuzingatia usafi katika Soko la Sabasaba na maeneo me...

Jiji la Dodoma laweka mkakati wa kudhibiti msongamano wa Bajaj na Daladala Stendi ya Mnada mpya

Image
Na. Mwandishi wetu, KIZOTA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeanza kuchukua hatua za kuboresha matumizi ya Kituo cha Mabasi Mnada Mpya kilichopo Kata ya Kizota kwa kuhakikisha daladala na bajaji zinaingia ndani ya kituo hicho wakati wa kupakia na kushusha abiria, badala ya kusimama nje ya kituo.   Hatua hiyo inalenga kuweka utaratibu katika eneo hilo, kupunguza msongamano wa vyombo vya usafiri pamoja na kuimarisha usalama na urahisi wa huduma kwa wananchi wanaotumia kituo hicho.   Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Stendi ya Mnada Mpya iliyopo Kata ya Kizota, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alisisitiza umuhimu wa halmashauri kuhakikisha kituo hicho kinatumika kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.   Senyamule alielekeza daladala na bajaji kuingia ndani ya kituo wakati wa kupakia na kushusha abiria, akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuboresha mtiririko wa usafiri na kuhakikisha mazingira ya kituo yanakuwa sal...

Halmashauri ya Jiji la Dodoma yafanyia marekebisho Barabara ya kuingia Stendi ya Mnadani, Kizota

Image
Na. Mwandishi wetu, KIZOTA Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea na zoezi la kufanya marekebisho ya barabara ya kuingia katika Stendi ya Mnadani Kata ya Kizota, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.   Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuzungumza na wamiliki wa daladala na bajaji jana, ambapo alisisitiza umuhimu wa vyombo hivyo kuingia na kupaki ndani ya stendi badala ya kusimama na kupaki nje ya eneo la stendi, hali ambayo ni kinyume na utaratibu na sheria zilizowekwa.   Halmashauri imeanza kuchukua hatua za haraka kuhakikisha mazingira ya kuingia na kutoka katika Stendi ya Mnadani, Kata ya Kizota yanakuwa rafiki na salama kwa daladala, bajaji, abiria na watumiaji wengine wa barabara.   Marekebisho hayo yanatarajiwa kurahisisha utekelezaji wa maelekezo hayo na kuhakikisha Stendi ya Mnadani Kata ya Kizota inatumika kwa utaratibu unaostahili, huku ikisaidia kupunguza msongamano n...