Posts

Showing posts from September 21, 2024

Jiji la Dodoma latoa Kilo 790 za sukari kwa shule 150

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetoa kilo 790 za sukari kwa ajili ya walimu wa shule za msingi na sekondari ili kuwawezesha kupata uhakika wa chai wanapokuwa shuleni ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini za kuhakikisha nishati safi ya kupikia inatumika katika taasisi mbalimbali. Kilo hizo zilitolewa na Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago wakati wa hafla ya ugawaji mitungi ya gesi na majiko 1,000 kwa shule, zahanati, vituo vya afya, vituo vya watoto yatima na mama na baba lishe tukio lililofanyika katika uwanja wa Nyerere square jijini Dodoma. Naibu Meya Chibago alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imechangia kilo 790 za sukari kwa shule za msingi na sekondari 150. Shule za msingi zilizopewa sukari hiyo ni 104 na shule za sekondari ni 46 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais wa Tanzania na mbunge wa jimbo la Dodoma mjini, aliongeza. Akiongelea zoezi la utoaji wa majiko na mitungi...

Wananchi wa Dodoma watakiwa kutumia nishati safi kupikia

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA   Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule aeleza faida za nishati safi kwa matumizi ya kupikia na kuwataka wananchi wa Dodoma kuacha kutumia nishati chafu kwa matumizi ya nyumbani na sehemu za kazi. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule aeleza faida za nishati safi Aliyasema hayo katika halfa ya ugawaji wa mitungi ya gesi na majiko 1,000 kwa shule, zahanati, vituo vya afya, vituo vya makao ya watoto na mama na baba lishe huku akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuimarisha matumizi ya nishati safi kwa ajili ya kupikia, kuboresha afya za watumiaji na kulinda mazingira. Alisema kuwa nishati safi ina faida kubwa kwa watumiaji na mazingira hatua hiyo inalenga kuimarisha matumizi ya nishati safi kwa ajili ya kupikia, kuboresha afya za watumiaji, na kulinda mazingira. “Faida za nishati safi ni pamoja na matumizi bila kuathiri afya za watumiaji. Pia, itapelekea hewa ya oksijeni kuongezeka na miti kuendelea kukua, na hivyo, Dodoma itaendelea kuwa salam...