Posts

Showing posts from August 2, 2025

TARURA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE NZUGUNI JIJINI DODOMA

Image
#Yajipanga kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu ushiriki wa vikundi vya kijamii katika matengenezo ya barabara nchini   Na. Mwandishi Wetu, DODOMA  Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inashiriki Maonesho ya Nane Nane kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Maonesho vya Nzuguni jijini Dodoma.  TARURA inashiriki maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu kazi na majukumu yake pamoja na kupokea maoni na malalamiko kutoka kwa wananchi. Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa TARURA, Catherine Sungura amesema kuwa TARURA imejipanga kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali wanayoyasimamia yanayohusu ujenzi wa miundombinu ya barabara nchini. Kwa mujibu wa Sungura baadhi ya maeneo hayo ni pamoja usimamizi wa matengenezo ya kawaida, matengenezo ya maeneo korofi shughuli za maabara,mazingira na jamii. "Kupitia wataalamu wetu ambao wapo katika banda letu tumejipanga pia kutoa elimu kwa wananchi na wadau wetu wengine namna wanavyoweza kus...

Fursa ya Ufugaji wa Mbwa katika Jiji la Dodoma

Image
                                                                 Na Eupilio Anthony, DODOMA Maonesho ya sherehe za wakulima nchini inazofahamika kama Nanenane, wananchi wajitokeza kujionea mifugo, bidhaa za kilimo, uvuvi na bidhaa zilizosindikwa na wajasiliamali kutokana na mazao hayo huku wakifurahishwa na ufugaji wa mbwa kisasa. Moja kati ya wafugaji na mfanyabiashara wa mbwa, Mwakaleli Mwakasege aliwaeleza wananchi anavyofanya biashara hiyo. “Mimi ni mfugaji wa mbwa kwa zaidi ya miaka 10 na leo kwenye sherehe hizi za Nanenane nimefurahi sana kuona jamii inaanza kutambua thamani ya mnyama huyu. Mbwa si tu mnyama wa kufuga kwa ajili ya ulinzi ni rafiki mkubwa wa familia, mlinzi wa mali, na kwa sasa, chanzo cha kipato kwa watu wengi kama mimi” alisema Mwakasege. Aliendelea kueleza tabia za mbwa anapoishi na binadamu ku...