Posts

Showing posts from February 23, 2025

Vilabu vya michezo vyashiriki mazoezi ya viungo vya mwili jijini Dodoma

Na. Aisha Ibrahim, Mailimbili-DODOMA Vilabu mbalimbali vya michezo jijini Dodoma, vimejitokeza kwa wingi katika Bonanza la “Dodoma Aerobics Festival” msimu wa kwanza, lililofanyika katika kiwanja cha Chinangali Park, kuanzia saa 12:00 asubuhi mpaka saa 6:00 mchana kwa lengo la   kuwakutanisha wanamichezo wote kushiriki mazoezi mbalimbali ya kuimarisha viungo vya mwili. Bonanza hilo liliandaliwa na kikundi cha wakufunzi wa michezo kutoka Jiji la Dodoma 'Dodoma Trainers Group' lilijumuisha mchezo wa kunyanyua uzito, kupasha mwili, kurukaruka na vikundi vya kukimbia. Akizungumza wakati wa bonanza hilo, mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, aliwasisitiza wana Dodoma kuendelea kufanya mazoezi kila siku hasa siku ya Jumamosi kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alivyosisitiza kila mtanzania kujitengea siku ya kufanya mazoezi kwa lengo la kuimarisha viungo vya mwili. “Mazoezi ni afya, mazoezi ni tiba hi...

Dodoma Jiji FC, Gari Limewaka

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imeichakaza Klabu ya Soka ya Fountain Gate FC, kwa kuichapa bao Moja kwa nunge katika mchezo wa Ligi kuu ya NBC Tanzania bara, mchezo uliopigwa katika dimba la Jamhuri hapo jana, bao pekee la Dodoma Jiji FC, liliwekwa kimiani na mchezaji Idd Kipagwile, kwa mkwaju wa penati mnamo dakika ya 37 ya mchezo. Baada ya mchezo kutamatika Kocha Mkuu wa Dodoma Jiji FC, Mecky Mexime alisema “niwapongeze wachezaji wangu kwa kupambana na kuhakikisha tunashida mchezo. Mchezo ulikua ni mgumu ukizingatia hatuna idadi ya wachezaji wengi wenye utimamu kimwili lakini wachezaji waliopo kwa uchache wao wameweza kuonesha umuhimu wao kwenye timu wamepambana kadri ya uwezo wao tumeweza kushinda mchezo, tumetengeneza nafasi kwa idadi kubwa sana kipindi cha pili lakini kutokana na presha ya mchezo tukashindwa kuzitumia lakini kwenye mchezo ujao tutajiandaa kwenda kuhakikisha tunatumia nafasi tunazotengeneza kwa usahihi”. Akiongelea malengo ya timu ...