Posts

Showing posts from December 23, 2023

Kata ya Chamwino yatekeleza agizo la RC la usafi wa Mazingira

Image
KATA ya Chamwino imetekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule la kufanya usafi kila jumamosi kwa lengo la kuliweka Jiji la Dodoma safi. Akiongelea utekelezaji wa agizo hilo, Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa usafi huo ulifanyika katika maeneo ya korongo la Mailimbili na Mwaja. Usafi huo ulihusisha kufyeka vichaka na nyasi, kuokota makopo na mifuko ya plastiki iliyozagaa katika korongo na kuzibua mitaro ya maji yenye urefu wa mita 100, aliongeza. Alisema kuwa kata yake ilitumia zoezi hilo la usafi wa pamoja kuwahimiza wananchi kufanya usafi wa mazingira katika maeneo ya biashara na makazi pamoja na kuhakikisha wanatunza mazingira katika msimu huu wa sikukuu. Usafi wa pamoja katika Kata ya Chamwino ulishirikisha Afisa Mtendaji Kata, Wenyeviti wa mitaa, mabalozi na wananchi.  

WAZIRI SILAA ASIMAMISHA MATUMIZI YA KITUO CHA MAFUTA CHA BARREL DAR ES SALAAM

Image
Na Eleuteri Mangi, WANMM   Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amesimamisha matumizi ya Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni jijini Dar es salaam na kupiga marufuku ujenzi holela wa vituo vya mafuta nchi nzima vinavyojengwa kwenye makazi ya watu hatua inayohatarisha usalama wa watu na mali zao.   Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa akiozungumza na wananchi wa Mikocheni wakati akisimamisha matumizi ya Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni Desemba 23, 2023 jijini Dar es salaam Waziri Silaa ametoa agizo hilo Desemba 23, 2023 alipoenda kukagua eneo kilipojengwa kituo hicho na aliambatana na Kamati ya ulizi na usalama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam.   "Kufuatia agizo hili, nawaagiza Wakuu wote wa Idara ya Ardhi na Mipango Miji nchi nzima wafanye uhakiki wa vituo vya mafuta kwa maana ya viwanja, mabadiliko ya matumizi ya ardhi, mchakato uliotumika, ukubwa wa viw...

WIZARA YA ARDHI YAZINDUA MFUMO RASMI WA KUWAHUDUMIA WANANCHI “ARDHI APP”

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imezindua mfumo rasmi wa kuwahudumia wananchi popote walipo kupitia simu ya kiganjani “Ardhi App” wa kuwasilisha malalamiko ama migogoro ya ardhi katika wizara hiyo.   Akizindua mfumo huo  Desemba 22, 2023 jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wake na Wahariri wa Vyombo vya Habari kupitia Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Waziri  wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa  amesema, mfumo huo ni rafika na utawarahisishia wananchi kupata huduma wakiwa katika maeneo yao popote walipo. “Mfumo huu wa “Ardhi App” utakuwa msaada mkubwa sana kwa wananchi wetu, utapunguza gharama na muda wa wananchi kupata huduma katika maeneo mbalimbali nchini, badala yake mwananchi atapata huduma za ardhi kiganjani mwake” amesema Waziri Silaa. Kwa mujibu wa Waziri Silaa, mfumo huo pia utawasaidia wananchi kutoa mrejesho wa ubora wa huduma walizopatiwa pamoja na kuwasilisha tena malalamiko husika pale ambapo hawajaridhika...