Posts

Showing posts from September 14, 2025

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini ni nyenzo ya utendaji kazi serikalini – Dkt. Biteko

Image
Na. Mwandishi Wetu, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amehitimisha Kongamano la Nne la Kitaifa la Ufuatiliaji, Tathmini na Kujifunza lililofanyika jijini Mwanza akiweka mkazo kuwa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha kuwa kila taasisi inatimiza wajibu wake kwa ufanisi na hivyo kufikisha huduma bora kwa wananchi. Kutokana na hilo, Dkt. Biteko amewataka Wataalam wa Ufuatiliaji na Tathmini nchini kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu bila kuogopa kuchukiwa kwani taifa linawategemea ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi. “Hakuna mtu au taasisi inayoweza kufanikisha majukumu yake bila kufanya tathmini, ninyi ndio mnaoweza kutambua changamoto mapema na kuzitafutia suluhisho kabla hazijawa kubwa, taasisi yoyote inayokosa mfumo huu inafanana na timu inayoingia uwanjani bila refa..” alisema Dkt. Biteko. Alitoa mfano kuwa katika sekta ya umeme, kabla ya kupeleka huduma hiyo eneo lolote lazima tathmni ifanyike ili kuepuka kurudia...

OCPD yapongeza ushirikiano na Ofisi ya Mashitaka katika zoezi la Urekebu wa Sheria

Image
Na. Calvin Gwabara, DODOMA Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) imekabidhi Juzuu za toleo la Urekebu wa Sheria la Mwaka 2023 kwa Ofisi ya Taifa ya Mashitaka na kupongeza mchango mkubwa uliotolewa na Ofisi hiyo kupitia watumishi wake kwenye utekelezaji wa zoezi la Urekebu.  “Wakati tunaanza zoezi hili Ofisi yetu ilikuwa na changamoto kubwa ya uhaba wa watumishi hasa Mawakili wa kufanya kazi hii lakini tulikuwa tukibisha hodi kwenye Ofisi yako kuomba Mawakili kuja kushirikiana nasi katika kutekeleza zoezi hili, na hakika walitusaidia sana hadi tumekamilisha” alieleza Katuga. Aliongeza “Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria kwa kutambua mchango wenu imeona ni muhimu na Ofisi yako pia ipate nakala hizi ingawa tunatambua kuwa tumeleta chache kutokana na gharama lakini ziwasaidie kwa kuanzia na kuwa kama kumbukumbu kwenu, lakini mnaweza kupata nakala laini zote kupitia mfumo wa OAG MIS library” alieleza Katuga. Kaimu Mkurugenzi huyo wa Divisheni ya Urekebu, Tafiti na Mafunzo ameong...

Ruzuku ya Mil. 250 yatolewa kwa wabunifu wa matumizi ya bora ya Nishati

Image
*Kamishna wa Umeme asema Serikali itaendelea kuwawezesha vijana wabunifu katika teknolojia ya matumizi bora ya nishati  *Wabunifu wa kike wapongezwa kujitokeza kwa wingi matumizi bora ya nishati nchini   Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya (EU) na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP), imetoa ruzuku ya jumla ya shilingi milioni 250 kwa wabunifu kumi waliofanya vizuri katika Mashindano ya Ubunifu na Ufanisi wa Matumizi Bora ya Nishati. Kamishna wa Umeme na Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Innocent Luoga amekabidhi ruzuku hiyo akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mha. Felchesmi Mramba katika hafla iliyofanyika Septemba 12, 2025 jijini Dar es Salaam.  Hafla hiyo iliwakutanisha wabunifu mbalimbali waliobobea katika nyanja ya ufanisi wa matumizi bora ya nishati katika maeneo matatu ambayo ni ubunifu kwenye vifaa vinavyotumia umeme kidogo, ubunifu kwenye miundombinu ya majengo yanayotumia umeme kidogo pa...

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali yawaasa wahariri wa vyombo vya habari kutumia kalamu kulinda amani ya taifa

Image
Na. Noel Rukanuga, DODOMA Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imewataka wahariri wa vyombo vya habari nchini kutumia kalamu zao kwa uadilifu, kwa kuzingatia maadili ya taaluma na kuhakikisha wanahabarisha umma kwa namna inayolinda amani na usalama wa taifa. Akizungumza wakati akifunga kikao kazi cha siku mbili kati ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wahariri wa vyombo vya habari, kilichofanyika leo Septemba 12, 2025 katika Ukumbi wa Mkemia Mkuu wa Serikali, jijini Dodoma, Mkurugenzi Msaidizi wa Uratibu na Huduma za Ushauri wa Kisheria, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Ipyana Mlilo, amesema kuwa sekta ya habari ni mhimili muhimu katika maendeleo ya taifa, hivyo kikao kazi hicho kimetoa nafasi ya kuimarisha ushirikiano baina ya wahariri na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, ili kuendelea kutoa elimu ya kisheria kwa jamii kwa weledi. “Kikao hiki kimekuwa na manufaa makubwa katika kuhakikisha jamii inapata uelewa mpana kuhusu masuala ya kisheria. Tumejadiliana mambo mengi ...

Madereva wa Serikali wahimizwa kuendesha kwa ustadi, kulinda Usalama barabarani

Image
  Na. Sizah Kangalawe, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amewahimiza madereva wa Serikali kutumia vyema mafunzo waliyopatiwa katika kuboresha utendaji kazi wao na kuleta tija zaidi. Alitoa maagizo hayo Septemba 04, 2025 jijini Dodoma wakati akifunga Kongamano la Nne la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania (CMST) lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete. "Naamini mada mlizofundishwa hapa zitakwenda kuboresha uwezo wenu katika utendaji kazi na kuleta tija zaidi katika kuhakikisha mwajiri mkuu ananufaika na mafunzo mliyopata kupitia kongamano hili, na ninaamini kuwa kushiriki kwenu kutapelekea kuendesha magari kwa ustadi na kupunguza matukio ya ajali. Tutajua thamani ya abiria mliowabeba na kuendesha tukiwa tunawakinga na madhara, lakini pia mtajua thamani ya vitu mnavyobeba kupitia magari hayo ambayo mnatakiwa mvisafirishe kwa usalama,” alisema Senyamule. Alifafanua kuwa madereva wa Serikali ni mhimili muhimu katika utekelezaji wa majukumu y...

ACC yatoa vifaa vya Mil. 62 kwa watoto wenye changamoto ya Afya

Image
Na. Sofia Remmi, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amepokea na kukabidhi vifaa vya michezo, vya kujifunzia pamoja na vitendea kazi vya watoa huduma za afya ngazi ya Jamii ili viweze kuwafikia walengwa waliopo katika baadhi ya halmashauri za mkoa huu. Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jengo la Mkapa. Akizungumza na baadhi ya wadau na watoa huduma ngazi ya jamii amesema Mkoa unashirikiana na Shirika la Action for Community Care (ACC) katika kutekeleza miradi ya Imarisha Afya na ViiV Pediatric Breakthrough Partnership ambayo inalenga kusaidia watoto na vijana wanaoishi na Virusi vya UKIMWI wenye umri wa miaka 0-19. Miradi inawezesha kuwaibua na kuwaunganisha watoto na vijana kwenye matibabu, kuwasaidia kubaki katika huduma na matibabu na kuishi maisha yenye afya. “Vifaa vya  michezo na vya kujifunzia vinavyopokelewa leo vina umuhimu wa kipekee kwa kuwa  vitawezesha uchangamshi na ukuaji wa ubongo wa watoto na kuwa...