Posts

Showing posts from January 23, 2025

Ujenzi wa Kituo cha Afya Zuzu wafikia 98%

Image
Na. Dennis Gondwe, ZUZU UJENZI wa Kituo cha Afya Zuzu umefikia asilimia 98 ya utekelezaji kikitarajiwa kuhudumia wananchi 10,054 kwa kuwahakikishia huduma bora za afya na kuwaondolea hadha ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya. Kauli hiyo ilitolewa na Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Goodluck Magoti alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Zuzu kwa Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho. Magoti alisema “kutokana na changamoto ya kukosa huduma za Kituo cha Afya katika Kata ya Zuzu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilianza ujenzi wa Kituo cha Afya Zuzu ili kusogeza huduma za matibabu mbalimbali karibu na wananchi. Halmashauri ilitoa kiasi cha shilingi 299,439,348,54. Hadi kufikia sasa kiasi cha shilingi 285,4439,000,54 zimetumika kwa ujenzi wa majengo ya Wagonjwa wa Nje (OPD) na Maabara na kubakiwa na shilingi 14,000,348.54 kwa ajil...

DC Shekimweri ahimiza usafi kudhibiti magonjwa Dodoma

Image
  Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri aliitaka jamii kuzingatia suala la usafi wa mazingira katika maeneo yao ili kujikinga na magonjwa na kufanya mji kuwa safi na salama katika kipindi hiki cha maandalizi ya bajeti ya halmashauri ili wananchi wawe na afya bora. Aliyasema hayo katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kupokea na kujadili mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa fedha 2025/2026. Alhaji Shekimweri alisema “ wenzetu maafisa afya, watendaji wa kata, changamoto za uchafu wa mji wetu ni usimamizi kwa sehemu fulani, yapo maeneo ya kampuni za usafi, yapo maeneo yanavikundi vya usafi, lakini ni wajibu wa mwananchi mmoja mmoja kufanya usafi wa eneo lake. Kwahiyo, tuimarishe usimamizi, na kuna makampuni na vikundi na vinalipwa kwa kufanya kazi hizo ” . Akiongelea suala la usalama katika Halmashauri y...

Dodoma Jiji U-20 yakita Kambi Kileleni

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya soka ya Dodoma Jiji chini ya umri wa miaka 20 (U-20) imeendeleza ubabe kwa wapinzani wake wanaoshiriki ligi ya vijana ya NBC chini ya umri wa miaka 20 Tanzania bara baada ya kuwashushia kichapo cha mabao 2-1 wanajeshi wa mpakani Mashujaa FC U-20, katika mchezo uliovulumishwa katika nyasi za dimba la Jamhuri Dodoma hapo jana. Baada ya mchezo kutamatika kocha wa Dodoma Jiji U-20, Jeremiah Chido alisema “ mchezo umemalizika salama na tumepata kitu ambacho tulikua tunakihitaji ambacho ni alama tatu muhimu. Alama ambazo zinatufanya tuendelee kuwa kileleni katika kundi letu na kutufanya tusicheze kwa presha michezo inayokuja mbele yetu, michezo ambayo tutakuwa ugenini ”. Katika hatua nyingine Chido akaweka wazi malengo yao kwenye msimu huu wa Ligi ya Vijana ya NBC Tanzania Bara. “ Malengo yetu msimu huu ni kuchukua ubingwa kwasababu msimu uliopita tulifika fainali ila bahati haikuwa upande wetu. Kwahiyo, msimu huu tukishirikiana halmashauli, mashabiki...

Prof. Mwamfupe; Taka ni fursa ya kutengenezea mbolea

Image
  Na. Aisha Haji, DODOMA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe, amewataka wananchi kuendelea kutunza mazingira na kutumia takataka zinazotokana na mazao kama fursa ya kutengeneza mbolea ili kuweza kuinua sekta ya kilimo na uchumi wa halmashauri kiujumla. Aliyasema hayo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakati wa majadiliano na Kamati ya Ushauri ya Wilaya iliyokutana kupitia mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Akizungumza kuhusu umuhimu wa mbolea zitokanazo na takataka za mazao, alisema kuwa taka za mazao ambazo zinaoza kwa urahisi ni fursa nzuri sana ya kiuchumi kuweza kutengeneza mbolea. Pia alidokeza kuwa halmashauri imejipanga katika suala la kutoa mikopo, mafunzo na ushauri wa kitaalamu kwa wananchi kuhusu namna ya kutumia taka zitokanazo na mazao kwa ajili ya kutengeneza chakula cha kuku kwa kufuata utaratibu maalumu. Prof. Mwamfupe alisema “halmashauri itak...