Posts

Showing posts from September 15, 2026

AI Ultrasound kuokoa maisha ya Mama na Mtoto Dodoma

Image
Na. Lulu Luvanda, MKONZE Mkoa wa Dodoma umechaguliwa kuwa mkoa wa majaribio katika matumizi ya teknolojia ya AI Ultrasound, kupitia Mradi wa The Study of AI-Facilitated Ultrasound Feasibility and Assessment of Resources and Integration (SAFARI Project), unaolenga kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto. Hatua hiyo imekuja wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya AI Ultrasound kwa vituo 32 vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Dodoma, iliyofanyika katika Kituo cha Afya Mkonze, jijini Dodoma. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alikipongeza   Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa kuendelea kufanya tafiti zenye uhalisia na zinazolenga kutatua changamoto mbalimbali katika jamii, ikiwemo tafiti katika sekta za Utalii, Mazingira pamoja na Lishe. Alisema kuwa matumizi ya vifaa hivyo katika vituo vya afya yatawezesha wananchi kupata huduma za awali kwa ukaribu zaidi, hivyo kupunguza changamoto ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za uchunguzi...

Wanafunzi watakiwa kujua umuhimu wa utunzaji Mazingira Dodoma Makulu

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA MAKULU   Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sechelela jijini Dodoma wamepata elimu kuhusu umuhimu wa utunzaji na uhifadhi wa mazingira, ikiwa ni sehemu ya kuwajengea uelewa na kuhamasisha ushiriki wao katika shughuli za maendeleo ya jamii.   Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Maendeleo ya Jamii Kanda ya utoaji huduma Namba Nne, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mariam Nyirenda, amesisitiza umuhimu wa kila mmoja kuwa na jukumu katika kulinda mazingira.   Amewahimiza wanafunzi kushiriki katika shughuli za usafi, upandaji miti na uhifadhi wa mazingira kwa ajili ya afya na ustawi wa jamii.   Aidha, amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa mazingira katika shule, familia na jamii kwa ujumla, kwa kuhamasisha wengine kuchukua hatua katika kuyatunza.   Kwa upande wake Dorcas Alex, Mwanafunzi    alisema kuwa wanafunzi wanashiriki usafi wa mazingira kwa lengo la kuhakikisha wanasoma katika maeneo masafi   Ujumbe huo una...

Kata ya Ipala yatekeleza agizo la usafi wa Mazingira

Na. Mwandishi wetu, IPALA   Zoezi la uhamasishaji wa Usafi wa Mazingira katika Kanda Namba Saba limekua lenye mafanikio makubwa. Zoezi hilo limefanyika katika mitaa mitano iliyopo ndani ya Kata ya Ipala Mtaa wa Sokoine, Madukani, Azimio, Ukombozi na Mwinyi.   Usafi wa Mazingira ulishilikisha wataalamu kutoka Kanda Namba Saba, wenyeviti wa mitaa, Diwani pamoja na wananchi waliojitoa kusafisha mitaa yote mitano kwa ushirikiano mkubwa kufuatia agiza la Mkuu wa Mkoa wa Dodoma la kusafisha Jiji la Dodoma kila siku.   Akizungumza baada ya zoezi la Usafi wa Mazingira, DIwani wa Kata ya Ipala, Andrew Muhulo aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo la usafi wa Mazingira na kuwasihi wasiishie hapo tu maana zoezi la usafi ni maisha ya kila siku ya mtu mmoja mmoja.   “Niwapongeze wananchi wote kwa kujitokeza kwenu kwa wingi mkuu wetu wa mkoa amesema zoezi la usafi ni la kila siku hivyo tudumishe usafi katika maeneo yote na viongozi kutoka ...

Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kufungua fursa za kiuchumi kwa Vijana Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesema itaendelea kufungua na kuwawezesha vijana kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwawezesha kujitegemea. Akizungumza kuhusu shughuli zitakazotekelezwa katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, Afisa Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Ndulani alisema kuwa moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni kuwawezesha vijana kupata fursa za kiuchumi.   Aliongeza kuwa fursa hizo ni pamoja na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa wafanyabiashara wadogo, maarufu kama machinga.   “Halmashauri pia itaendelea kutoa elimu ya ujasiriamali na stadi mbalimbali kwa vijana ili kuwajengea uwezo wa kutumia fursa zinazopatikana na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi,” alisema Ndulani.   Aliongeza kuwa Halmashauri itaendelea kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Vijana pamoja na kuwaunganisha vijana ...

Maadhimisho ya Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kutilia mkazo usafi Dodoma

Image
Na. Lulu Luvanda,  DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeandaa kampeni ya kuhamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa usafi katika Maadhimisho ya Mwezi wa Maendeleo ya Jamii yanayofanyika jijini Dodoma Mwezi Septemba, 2026 kwa lengo la kuimarisha ushiriki wa jamii katika kutunza mazingira. Akizungumza kuhusu maandalizi ya maadhimisho hayo Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Charity Sichona, alisema kuwa  wananchi watapewa elimu ya namna ya kuchangia katika utunzaji wa mazingira bora kupitia tabia sahihi za kila siku. Alisema kuwa moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni usimamizi wa taka ngumu, ambapo wananchi wataelimishwa kuhusu namna ya kuzihifadhi na kuzitenganisha kulingana na aina zake kuanzia zinapozalishwa. Kwa mujibu wa Sichona kutenganisha taka katika chanzo kutarahisisha ukusanyaji na uendeshaji wa taka, huku taka zinazoweza kutumika tena zikipata nafasi ya kurejelewa badala ya kuishia katika maeneo yasiyokusudiwa. Ali...

Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kujikita kutoa elimu ya Bima ya Afya Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya, ikiwa ni sehemu ya shughuli zinazofanyika katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii. Akizungumza kuhusu elimu hiyo, Mratibu wa Mfuko wa Afya ya Jamii Iliyoboreshwa (iCHF) wa Jiji la Dodoma, Patrick Batimo, alisema kuwa wananchi wanapatiwa elimu kuhusu bima ya afya, ikiwemo Mfuko wa Afya ya Jamii Iliyoboreshwa (iCHF) pamoja na Bima ya Afya kwa Wote. “Elimu hiyo inalenga kuwawezesha wananchi kuelewa umuhimu wa bima ya afya na namna wanavyoweza kupata huduma za afya kupitia mifumo hiyo”, alisema Batimo.   Aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kutumia fursa ya elimu inayotolewa ili kufahamu aina mbalimbali za bima ya afya, huduma zinazopatikana pamoja na umuhimu wa kuwa na bima wakati wanapohitaji matibabu. Aidha, utoaji wa elimu hiyo ni sehemu ya juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhakikisha wananchi wanafahamu huduma za bima ya afya na umuhimu wa kuji...

Wananchi kupatiwa elimu ya fursa za kiuchumi na mikopo ya 7%

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi na mikopo inayotolewa kupitia mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya shughuli za Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, unaolenga kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi na kupunguza umaskini. Akizungumza kuhusu shughuli za uwezeshaji zinazotekelezwa katika kipindi hicho, Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji na Kupunguza Umaskini, Hidaya Mizega alisema kuwa wananchi wanaendelea kupewa elimu kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi, namna ya kuzifikia na kuzitumia kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao. “Elimu hiyo pia inalenga kuwafahamisha wananchi kuhusu mikopo inayotolewa na halmashauri, ikiwemo mikopo yenye riba ya asilimia saba kwa wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga, ili kuwawezesha kukuza biashara zao na kuongeza kipato,” alisema Mizega. Aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kutumia fursa hizo kwa maendeleo yao, huku akisisitiza umuhimu wa ...

Jiji la Dodoma laimarisha huduma za Kilimo na Mifugo

Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamepokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kilimo na mifugo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, ikiwemo utoaji wa chanjo, utambuzi na usajili wa mifugo, ukaguzi wa nyama na ‘Agrovet’, pamoja na udhibiti wa visumbufu vya mazao.   Akizungumza katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero, alisema kuwa katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 na 2025/2026, halmashauri ilitekeleza shughuli mbalimbali za kilimo na mifugo kwa lengo la kuongeza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuboresha huduma kwa wananchi.   Alisema kuwa shughuli hizo zilihusisha utoaji wa chanjo kwa mifugo, utambuzi na usajili wa mifugo kwa kutumia hereni za kielektroniki, uhamasishaji wa msimu wa kilimo pamoja na udhibiti wa wadudu na magonjwa katika mazao ya bustani na zabibu.   “Katika kipindi hiki, tumetekeleza shughuli mbalimbali za kilimo na mifugo kwa lengo la ...