Posts

Showing posts from February 2, 2024

Wanasheria waanza mwaka mpya wa Mahakama

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alizindua rasmi mwaka mpya wa Mahakama 2024 na kuwatakia wanasheria wote kheri ya mwaka mpya wa mahakama ulioanza Februari 1, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na majaji wa Mahakama ya Rufaa Kauli hiyo aliitoa katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika bustani ya mapumziko Chinangali jijini Dodoma. ā€œTunaanza rasmi mwaka wa Mahakama na tunawakumbusha kuwa na mchango katika utendaji kazi kwa wadau wote wa Mahakama nchini, na nawakumbusha kufanya kazi kwa kuzingatia viapo vyenu vya utendaji kazi mlivyo viapa wakati wa kuanza kazi hiiā€ alisema Dkt. Samia Suluhu Hassan. Aidha, aliongezea kwa kuwapongeza watumishi wote wa Mahakama kwa kufanya kazi nzuri kwa kuendelea kutekeleza majukumu yao. ā€œNawapongeza sana waheshimiwa Mahakimu, wasajili wa mahakama kuu, majaji wa mahakama za rufaa na watumishi ...

Wizara yatakiwa kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi

Image
Na. Josephina Kayugwa, DODOMA Wizara ya Katiba na Sheria yatakiwa kutekeleza kikamilifu msaada wa kisheria kwa wananchi kwa lengo la kutenda haki. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongea na mamia ya wanasheria na wananchi Hayo yalisemwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika bustani ya mapumziko ya Chinangali yakiongozwa na kaulimbiu inayosema ā€˜Umuhimu wa dhana ya haki kwa ustawi wa Taifa, Nafasi ya Mahakama na wadau katika kuboresha Mfumo Jumuishi wa Haki Jinai’. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alisema taasisi zote za kisheria zinatakiwa kushirikiana katika jambo la kutenda haki kwa jamii na kuimarisha mfumo wa haki hii ni kutokana na kucheleweshwa na mashauri ambayo yanatakiwa kutekelezwa mapema. ā€œMuda wa mashauri ya kimahakama unatakiwa kupunguzwa ili kuwapa nafasi wananchi kwaajili ya kuendelea kutekeleza mambo mengine ya kimaendeleo na majaji wot...

Wanasheria watakiwa kufuata misingi ya Uadilifu

Image
Na. Arafa Waziri, DODOMA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwataka wanasheria nchini kufanya kazi kwa kufuata misingi ya uadilifu na kutenda haki.   Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongea katika maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini Aliyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika jijini Dodoma na kuwataka wanasheria wote nchini kufanya kazi kwa uadilifu mkubwa na kutenda haki kwa wananchi. ā€œMnalazimika kusimama katika misingi ya dini pamoja na Katiba ya Tanzania. Mna dhima mbinguni na Duniani kwahiyo, mna wajibu wa kutenda haki ili kuweka amanikwa wananchiā€ alisema Dkt. Hassan Lakini pia aliwapongeza wanasheria kuendelea kufanya kazi ya kusaidia wananchi kupata haki na kuwasisitiza kuwa na ushirikiano baina yao ili kubaini mapungufu yaliyopo na kuchukua hatua kwa pamoja. ā€œNiwapongeze kwa namna mnavyoendelea kutimiza majukumu yenu na hii ni ushahidi tosha kwamba mnafanya kazi kubwa na kwamba Mahakama inakwenda...