Posts

Showing posts from October 3, 2023

WILAYA YA DODOMA ILIKUSANYA 44,454,939,022 MWAKA 2022/2023

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma ilikusanya mapato ya shilingi 44,454,939,022 kupitia mifumo ya kieletroniki na kutekeleza miradi ya maendeleo katika mwaka wa fedha 2022/2023. Taarifa hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Chamwino jijini hapa. Ukusanyaji wa k odi na m apato kwa mfumo wa TEHAMA umeendelea kuimarika. “ Mheshimiwa Rais; w ilaya kwa mwaka wa fedha 2022/ 20 23 ilifanikiwa kupata m ashine za kielektroniki za kukusanyia mapato ( POS ) 304 na shilingi 44,454,939,022.82 zilikusanywa na kutumika kwenye miradi ya maendeleo ” alisema Mbugi . Kuhusu sekta ya biashara alisema malipo yote yanafanyika kupitia benki. “ Mheshimiwa Rais; Wilaya ya Dodoma imefanikiwa kusajili wafanyabiashara kwenye mfumo wa s erikali za m itaa wa ukusanyaji m apato na mali...

SHILINGI 9,539,477,529 ZACHANGIA KUONGEZA UFAULU DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma ilipokea shilingi 9,539,477,529 kwa ajili ya maendeleo zilizotumika kujenga miundombinu ya elimu msingi na sekondari na kuchangia katika ukuaji sekta hiyo na kuongeza ufaulu. Taarifa hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Chamwino jijini hapa. Mbugi alisema “ Mheshimiwa Rais; k atika kipindi cha Julai 2022 hadi Juni 2023, Wilaya ilipokea shilingi 9,539,477,529.06 kwa ajili ya maendeleo ya s ekta ya e limu.   Kati ya fedha hizo, shilingi 3,456,608,415.29 za e limu bila malipo kwa s hule za m singi na s ekondari na shilingi 6,082,869,113.77 zilitumika kujenga miundombinu katika s hule za m singi na s ekondari ” . Akiongelea uboreshaji mazingira ya kujifunzia na kufundishia alisema kuwa yameboreka. “ Mheshimiwa Rais; kuboreshw...

WILAYA YA DODOMA IMEPANDA MITI 4,500,000 KAMPENI YA KIJANISHA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA Dodoma imefanikiwa kupanda miti 4,500,000 katika kampeni ya Dodoma ya kijani na utekelezaji wa ujumbe wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 unaosisitiza utunzaji wa Mazingira. Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Abdalla Shaib Kaim akipanda mti kwenye mradi wa Maji safi nzuguni Akisoma risala ya utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Chamwino, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alisema kuwa Wilaya ya Dodoma ipo mstari wa mbele katika kutunza Mazingira. “K atika kutekeleza u jumbe wa Mwenge wa Uhuru wilaya imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali katika utunzaji wa Mazingira na kuokoa vyanzo vya Maji kwa ustawi wa viumbe hai na uchumi wa Taifa. Katika kipindi cha miaka mitano ya Kampeni ya Dodoma ya Kijani Miti 4,500,000 imepandwa katika maeneo mbalimbali pamoja na chanzo cha Maji Mzakwe. Aidha, w ilaya imeweza kusambaz...

MWENGE WA UHURU WAZINDUA KITUO CHA AFYA NKUHUNGU- DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, NKUHUNGU MWENGE wa Uhuru mwaka 2023 umezindua Kituo cha Afya Nkuhungu ili kiweze kuwahudumia watanzania baada ya kujiridhisha na ujenzi wa kituo hicho na nyaraka kufuatia ukaguzi uliofanyika. Kauli hiyo ilitolewa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, Abdalla Shaib Kaim alipoongoza Mwenge wa Uhuru kutembelea na kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya Nkuhungu kilichopo jijini Dodoma. Kaim alisema kuwa Mwenge wa Uhuru umepita kwenye Kituo cha Afya Nkuhungu na kusema kuwa ujenzi wake umefanyika vizuri. “Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya pamoja na maelekezo ambayo nimetoa kwa dhati kabisa na kwa heshima ya Mheshimiwa Rais na wananchi hawa niseme Mwenge wa Uhuru mwaka huu tumeridhia uzinduzi wa kituo hiki cha afya” alisema Kaim. Akisoma taarifa ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nkuhungu kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Dkt. Andrew Method alisema kuwa halmashauri inatekeleza mradi huo kupitia mapato ya nd...

SERIKALI YAPONGEZWA KUTOA FEDHA UJENZI WA DODOMA ENGLISH MEDIUM

Image
Na. Dennis Gondwe, IPAGALA KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, Abdalla Shaib Kaim ameipongeza serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo elimu nchini. Pongezi hizo alizitoa alipoongoza Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 kutembelea, kukagua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English Medium katika Kata ya Ipagala jijini Dodoma. Kaim alisema “niipongeze serikali ya awamu ya sita kwa kazi kubwa inayofanya ikiwa ni pamoja na kutenga na kutoa fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo. Tumejiridhisha na nyaraka za mradi huu baada ya kuzikagua zipo vizuri sambamba na mradi nikiri mpaka hatua hii kazi kubwa na nzuri imefanyika. Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 tumeridhia uwekaji jiwe la msingi” alisema Kaim. Akisoma taarifa ya ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi ya Dodoma English medium kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Mkuu wa Divisheni ya Elimu ya Awal...

WINGI WA WANANCHI NZUGUNI WAMKOSHA MKIMBIZA MWENGE KITAIFA UWEKAJI JIWE LA MSINGI BARABARA YA TARURA

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023, Abdalla Shaib Kaim amefurahishwa na mamia ya wananchi wa Kata ya Nzuguni waliojitokeza kwa wingi kuupokea na kuushangilia Mwenge wa Uhuru ulipofika kuweka jiwe la msingi mradi wa Barabara ya Nzuguni-Mahomanyika. Kaim alisema “kabla sijatoa majumuisho ya Mwenge wa Uhuru kukagua barabara hii niwapongeze wananchi wa Nzuguni kwa namna mlivyojitokeza kwa wingi, haya ni mafuriko makubwa, shamrashamra na vibe la kutosha kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru. Hakika ninyi ni watu wema na wazalendo wakubwa”. Aidha, alimpongeza Mbunge wa Jimbo la Dodoma, Anthony Mavunde kwa hamasa yake katika Mwenge wa Uhuru. “Pongezi kwa Mheshimiwa Mavunde tunakushukuru kwa kazi nzuri pamoja na wingi wa majukumu uliyonayo lakini umeona umuhimu wa kujumuika nasi. Hongera sana Mungu akubariki wewe ni mtu bingwa” alisema Kaim. Akiongelea mradi wa Barabara ya Nzuguni-Mahomanyika kilometa tano alisema kuwa imejengwa kwa kiwango bora....