Posts

Showing posts from April 14, 2025

Mikopo ya asilimia 10 yawang’arisha wajasiriamali Makutupora

Image
Na. Nancy Kivuyo, MAKUTUPORA Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia utoaji wa mikopo ya asilimia 10 yanufaisha makundi ya wanawake katika kujikwamua kiuchumi katika Kata ya Makutupora ikitajwa kuwa chachu ya kuinua maendeleo katika sekta ya kilimo, ufugaji na ujasiriamali. Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na makundi ya wanawake waliopata mikopo ya asilimia 10 katika Kata ya Makutupora, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Makutupora, Andrew Boma alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kusimamia vema uwezeshaji wa wananchi kupata haki zao hasa kwa makundi maalum ambayo yamewezeshwa kupitia mikopo hiyo. “Sisi Kata ya Makutupora vikundi 20 vimepatiwa mkopo wa jumla ya shilingi 230,000,000. Vikundi vya wanawake ni 10, vijana saba na watu wenye ulemavu vitatu. Mpaka sasa wameweza kurejesha shilingi 159, 980,000 na bakaa inaendelea kulipwa na vikundi hivyo” alisema Boma. Aliongeza kuwa vikundi hivyo vinajishughulisha na shughuli mbalimbali kama...

Kata ya Makutupora, kinara wa timu za michezo na ngoma za asili

Image
Na. Nancy Kivuyo, MAKUTUPORA Kata ya Makutupora yapongeza juhudi za serikali ya awamu ya sita za kuboresha miundombinu ya michezo jambo iliyopelekea hamasa kwa wananchi kupenda kushiriki katika michezo kwaajili ya kuibua vipaji na kuboresha afya zao. Pongezi hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Matukupora Hamis Jigwa mbele ya waandishi wa habari waliofanya mazungumzo nae baada ya kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa kwenye sekta ya michezo Kata ya Makutupora ina vikundi vya ngoma za asili ambavyo vimekuwa vikishiriki kwenye upokeaji wa Mwenge wa Uhuru na kushiriki mikutano ya kitaifa pamoja na timu za mpira wa miguu. “Hapa katani kwetu tupo vizuri, wananchi wa kata hii wanapenda michezo sana. Hata hii leo kuna mashindano yanaendelea, kama mtapata muda mtaona jinsi wananchi wa hapa wanavyojitokeza kwa wingi kushiriki katika michezo” alisema Jigwa. Akiongelea chachu ya hamasa ya michezo, alimtaja Rais, Dkt. Samia ...