Posts

Showing posts from November 16, 2024

Chigongwe watakiwa kujitokeza kupiga kura

Image
Na. Dennis Gondwe, CHIGONGWE WAKAZI wa Kata ya Chigongwe, Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba, 2024 ili waweze kuwachangua viongozi wanaowafaa. Masima Masima (wa pili kushoto) wakati wa kuhamasisha umma  Kauli hiyo ilitolewa na mkazi wa Kata ya Chigongwe, Masima Masima alipokuwa akiwahamasisha wananchi wa kata hiyo kujitokeza siku ya kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa alipopata nafasi ya kuhamasisha wakati timu ya uhamasishaji ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilipofika katani hapo kutoa hamasa kwa wananchi. Masima alisema “mimi binafsi cha kwanza, kupiga kura ni jukumu langu na ni haki yangu ya msingi. Tarehe 27 Novemba, mwaka huu ni siku ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Tunakwenda kumchagua mwenyekiti na wajumbe wake, mimi Masima nipo tayari kushiriki uchaguzi huo”. Kwa upande wa mkazi mwingine wa kata hiyo, Salome Nguji alisema kuwa wanachohitaji wapate kiongozi bor...