Posts

Showing posts from September 18, 2023

JIJI LA DODOMA LAPELEKA MIL. 20,000,000 KUMALIZIA MAABARA

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KUSINI HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepeleka shilingi 20,000,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la maabara katika Shule ya Sekondari Wella iliyopo Kata ya Kikuyu Kusini. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo katika hafla fupi ya kupokea vifaa vya maabara vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini. Kayombo alisema “Mheshimiwa mbunge hapa tayari unaona ujenzi unaendelea kwenye maabara yetu kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais, na sisi hatuwezi kukuangusha kwa sababu tunafanya kazi kwa kushirikiana. Tumeshaleta shilingi 20,000,000 hapa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maabara na inaenda kumaliziwa. Tunataka wanafunzi wetu waweze kufanya majaribio ya sayansi kwa vitendo. Mheshimiwa mbunge kwa maelekezo yako ya juzi ulituelekeza tutafute fedha na tumeshapata shilingi 8,000,000 kwa ajili ya kukamilisha matundu saba ya vyoo. Miongoni mwa changamoto am...

MBUNGE MAVUNDE AKABIDHI VIFAA VYA MAABARA VYA SH. 9,000,000/=

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KUSINI ELIMU ndiyo mkombozi kwa vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kuwasaidia kutoa mchango katika maisha yao na maendeleo ya taifa la Tanzania. Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde akiongea na mamia ya walimu, wanafunzi na wananchi waliojitokeza katika hafla ya kugawa vifaa vya Maabara  Kauli hiyo ilitolewa na Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini, Anthony Mavunde alipokuwa akiongea na wanafunzi na walimu wa shule za sekondari katika hafla ya kugawa vifaa vya maabara kwa ajili ya masomo ya sayansi tukio lililofanyika Shule ya Sekondari Wella iliyopo Kata ya Kikuyu Kusini. Mavunde ambae pia ni Waziri wa Madini alisema “elimu ninaamini kwamba ndiyo mkombozi wa kweli kwa vijana wetu na elimu hii itawasaidia kwenda kuwafanya wakatoe mchango wao na kulitumikia taifa la Tanzania na wao pia katika maisha yao. Baada ya kubaini tunachangamoto katika maabara zetu nyingi za vifaa, nikasema nianze na awamu ya kwanza na hii haitakuwa mwis...

MAANDALIZI UCHAGUZI MDOGO KATA YA NALA YAKAMILIKA

Na. Dennis Gondwe, Dodoma WANANCHI wa Kata ya Nala wametakiwa kutumia haki yao ya kidemokrasia kujitokeza kwa wingi kumchagua Diwani ili awawakilishe na kutetea maslahi yao. Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma mjini, John Kayombo alipotembelea na kukagua vituo vya kupigia kura katika Kata ya Nala. Kayombo alisema “maandalizi ya uchaguzi mdogo wa Kata ya Nala yamekamilika. Jumla ya vyama 11 vilichukua na kurejesha fomu na kupata nafasi ya uteuzi wa kugombea nafasi ya udiwani wa Kata ya Nala. Kwa upande wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ambayo mimi ndiyo Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Dodoma mjini na Kata ya Nala tumejiandaa vizuri na hatuna mapungufu yoyote”. Alisema kuwa jumla ya wapiga kura wanaopaswa kupiga kura ni 3,741.  “Niwaombe wananchi kujitokeza kwa wingi ili kutumiza haki yao ya msingi kumchagua mwakilishi wao ambae ni Diwani wa Kata ya Nala” alisema Kayombo. Kata ya Nala inafanya uchaguzi mdogo kufuatilia kifo cha aliyekuwa Diwani wa kat...