Posts

Showing posts from November 2, 2023

KISASA SEC YANUFAIKA NA UWEKEZAJI WA RAIS, DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA SHULE ya Sekondari Kisasa ni mnufaika wa uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya elimu na kuchangia kuongeza kiwango cha ufaulu. Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisasa, Mwl. Fredy Nyandoro alipokuwa akisoma taarifa ya shule Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisasa, Mwl. Fredy Nyandoro alipokuwa akisoma taarifa ya shule hiyo katika Mahafali ya 15 ya kidato cha Nne ya shuleni hapo. Mwl. Nyandoro alisema “ndugu mgeni rasmi, shule yetu tumekuwa na mafanikio kadhaa tangu kuanzishwa mwaka 2006. Mafanikio hayo ni kuongeza ufaulu mwaka hadi mwaka, kuongeza idadi ya watahiniwa na idadi ya vijana wanaojiunga elimu ya juu na vyuo vya kati imeongezeka. Shule imefanikiwa kuongeza miundombinu mwaka 2019 tulianza kujenga jengo la utawala na limekamilika. Mwaka 2021 tukapata mradi wa kuongeza madarasa kwa fedha za Uviko- 19 tulikuwa na madarasa matatu na kufanya madarasa kufikia ...

WAZAZI NI KIUNGO MUHIMU UFAULU WA WANAFUNZI KISASA SEC

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WAZAZI wa wanafunzi katika Shule ya Sekondari Kisasa wametakiwa kuwa kiungo muhimu baina ya walimu na wanafunzi katika malezi bora na kuwasaidia wanafunzi kufaulu. Mjumbe wa Bodi ya Shule ya Sekondari Kisasa, John Komba akiongea na Jumuiya ya Shule ya Kisasa Sekondari Kauli hiyo ilitolewa na Mjumbe wa Bodi ya Shule ya Sekondari Kisasa, John Komba kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo katika mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika shuleni hapo. Komba alisema “niwashukuru ninyi wazazi kwa kufika kwenu na kutoa ushirikiano kwa wanafunzi wetu kwa ajili ya kuwapatia elimu. Ninyi ni sehemu na msaada mkubwa kwa ajili ya kuwawezesha walimu waweze kutimiza majukumu yao ya kuwalea na kuwafundisha wanafunzi wanapokuwa shuleni. Na kwa wale wanaoshindwa kutimiza majukumu yao kama wazazi ndio usumbufu ambao walimu wanaupata kutokana na ushirikiano mdogo kati ya wazazi na walimu na kupelekea matokeo yasiyo mazuri kwa wanafunzi kuanzia malezi hadi taaluma. Niwaombe...