Posts

Showing posts from November 22, 2024

Wasimamizi vituo vya kupigia kura watakiwa kufanya kazi kwa weledi

Image
Na. Dennis Gondwe, MTUMBA WASIMAMIZI wa vituo vya kupigia kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na uzalendo wakizingatia kanuni na taratibu ili kuweza kufanikisha uchaguzi huo. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Dkt. Frederick Sagamiko wakati akifungua semina Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akifungua mafunzo kwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura, tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba. Dkt. Sagamiko alisema kuwa wasimamizi hao wapo kwa ajili ya kuapishwa na kupewa mafunzo kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kutokana na sifa na uwezo wao katika utendaji kazi ndiyo zimewafanya waweze kuchaguliwa. “Tunahitaji kuongeza umakini na usikivu wakati huu wa mafunzo. Hata kama ulisimamia uchaguzi uliopita, huu ni wa mwaka 2024 na haujawahi kufanyika popote. Hivyo, kuna utofauti kati ya...

Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura Waaswa kuviishi viapo vyao

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameaswa kuviishi viapo vyao walivyoapa ili wawe na muongozo mzuri pindi watakapokuwa katika vituo vyao vya kazi ifikapo tarehe 27 Novemba, 2024. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko wakati akifungua semina  Hayo yalisemwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akifungua semina ya wasimamizi wa vituo vya kupigia kura iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba. “Mtaenda kuapishwa, naomba mkaishi kiapo mtakachokipata, ili iwe dira na ndio yawe makatazo ya mambo ya kutokufanya wakati wa usimamizi” alisisitiza Dkt. Sagamiko. Akiongelea kuhusu kanuni na taratibu za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, aliwasisitiza wasimamizi wa vituo vya kupigia kura, kufuata kanuni za uchaguzi za mwaka huu 2...