Posts

Showing posts from June 8, 2025

Prof. Kabudi atoa salam za pongezi kwa wataalam walioshiri kutengeneza Sheria ya Mazingira

Image
Na. Nancy Kivuyo, Dodoma Waziri wa Habari, Sanaa, Michezo na Utamaduni, Prof. Palamagamba Kabudi amewasihi viongozi wenye mamlaka ya kusimamia Sheria ya Mazingira ngazi zote kuziweka katika utekelezaji ili utunzaji wa mazingira ufanikiwe kwa asilimia zote. Aliyasema hayo wakati akitoa salamu katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyofanyika jijini Dodoma katika ukumbi wa Jakaya Kikwete. Prof. Kabudi alisema kuwa utunzaji wa mazingira ni jambo mtambuka wananchi wote wanapaswa kulifahamu. Aliomba pia kuwatambua wataalam waliohusika katika utengenezwaji wa Sheria ya Mazingira. “Mheshimiwa Makamu wa Rais, na viongozi mliopo hapa, mimi pamoja na wataalam wa sheria tulishiriki mchakato wa kuandaa Sheria ya Mazingira ambao ulikua na safari ndefu, lakini tunashukuru tulifanikiwa kwa kiwango kikubwa na leo tupo hapa. Nawapongeza sana japokuwa kuna wenzetu kwa isivyo bahati wametangulia mbele za haki” alisema Prof. Kabudi. Aliongeza kuwa baada ya kuandaa sheria ile kish...

Dkt. Mpango ahimiza elimu kwa jamii juu ya utunzaji wa Mazingira

Image
Na. Nancy kivuyo, DODOMA Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango atoa rai kwa tasnia ya habari, taasisi na wananchi wote kushirikiana kutoa elimu kwa jamii juu ya utunzaji wa mazingira ili kupunguza madhara yatokanayo na uharibifu wa mazingira. Aliyasema hayo akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyofanyika jijini Dodoma katika ukumbi wa Jakaya Kikwete. Dkt. Mpango alisema kuwa suala la usimamizi wa mazingira ni la kipaumbele katika maendeleo ya nchi. “Waheshimiwa viongozi mliopo hapa, chanzo kikubwa cha uharibifu wa mazingira ni tabia ya watu na pia mabadiliko ya tabia nchi. Yote haya hasara yake kidunia ni makubwa sana, takriban dola bilioni 300-600 kila mwaka zinapotea. Kwa mantiki hiyo ili kupata mazingira safi lazima wote tuwajibike” alisema Dkt. Mpango. Aliongeza kuwa nchi yetu inapambana kuhakikisha kwamba kwa miaka ijayo taka za pastiki zitokomezwe kwa kiwango kikubwa. Taka hizi za plastiki zinatelekezwa...