Posts

Showing posts from August 27, 2026

TARURA Dodoma yatakiwa kukamilisha miradi kwa wakati

Na. Coletha Charles, NZUGUNI Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wametakiwa kukamilisha kwa wakati, miradi ya uboreshaji wa barabara yenye urefu wa kilomita 3.8 kwa kuzingatia ubora na thamani ya fedha ili iweze kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi wa Jiji la Dodoma.   Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo, ikiwa ni sehemu ya hatua za kukabiliana na athari za mvua za El Nino.   Alisema kuwa utekelezaji wa mradi huyo unapaswa kwenda sambamba na usimamizi madhubuti wa muda, ubora wa kazi na matumizi sahihi ya fedha, ili wananchi wa Jiji la Dodoma wanufaike na miundombinu hiyo kwa muda uliokusudiwa.   “Ninawasihi TARURA kuhakikisha mradi huu unakamilishwa kwa wakati na kwa kuzingatia viwango vinavyotakiwa, ili wananchi waweze kupata manufaa yaliyokusudiwa. Muhimu ni kuhakikisha fedha zinazotumika katika mradi huu zinatoa thamani halisi kwa wanan...

Bwawa kujengwa kudhibiti mafuriko Nzuguni

Na. Coletha Charles, NZUGUNI Ujenzi wa bwawa kubwa la kuhifadhi maji ya mvua pamoja na mtaro wenye urefu wa zaidi ya kilomita 3.6 umeanza kutekelezwa katika Uwanja wa Maonesho ya Nanenane wa Dkt. John Malecela, hatua inayolenga kudhibiti mafuriko katika eneo la Nzuguni na kuyageuza maji hayo kuwa fursa ya uzalishaji.   Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo katika Kata ya Nzuguni jijini hapa, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabiri Shekimweri alisema kuwa serikali imejipanga kukabiliana na changamoto ya mafuriko katika eneo hilo, huku ikilenga kutumia maji ya mvua kwa kilimo na uvuvi.   Alisema kuwa kwa wastani Dodoma hupokea mvua kati ya milimita 440 na 550 kwa mwaka, hivyo kuna umuhimu wa kuweka mifumo ya kuvuna na kuhifadhi maji badala ya kuyaacha yapotee.   “Bwawa hili litapokea na kuhifadhi maji yanayokusanywa kutoka maeneo yanayozunguka uwanja na hivyo kupunguza hatari ya mafuriko kwa wananchi wa maeneo jirani. Pia mpango huu um...

DC Shekimweri aagiza utambuzi wa kaya maeneo hatarishi

Na. Coletha Charles, NZUGUNI Idara ya Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Jamii, Madiwani, Watendaji wa Kata na Polisi Kata, wameagizwa kushirikiana na mamlaka nyingine kubaini kaya zinazoishi katika maeneo hatarishi, ikiwemo njia za asili za maji, yanayoweza kuhatarisha usalama wa maisha na mali za wananchi na kuzihamasisha kuhamia katika maeneo salama.   Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri katika Jengo la Utawala la Viwanja vya maonesho ya Nanenane vya Dkt. John Malecela Kata ya Nzuguni, wakati wa utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu kuchukua hatua za kuzuia na kupunguza athari za mvua za El Nino pamoja na mvua zitakazokuwa juu ya wastani.   Alisema kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa wakijenga katika njia za asili za maji, hususan wakati wa kiangazi, jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha na mali wakati wa mvua, ambapo maji hurejea katika mikondo yake ya kawaida.   “Ujenzi katika maeneo hatarishi...

DC Shekimweri aagiza kuzingatia usalama maeneo ya uchimbaji madini ujenzi

Na. Coletha Charles, NZUGUNI Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma imetakiwa kuandaa orodha ya maeneo yote yaliyotolewa vibali vya uchimbaji wa madini ya ujenzi, kubaini yaliyo katika matumizi, yaliyokamilisha shughuli za uchimbaji na yale ambayo hayajarejeshwa katika hali salama.   Agizo hilo limetolewa katika Ofisi ya Utawala viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri katika kikao cha maandalizi ya kukabiliana na athari za mvua za El Nino.   Alhaj Shekimweri alisema kuwa waendeshaji wa maeneo hayo wanapaswa kutekeleza mpango wa ‘Environmental Management Plan’ (EMP) iliyowekwa wakati wa utoaji wa vibali, ikiwemo kusawazisha na kurejesha maeneo hayo katika hali salama baada ya kumaliza uchimbaji.   “Tupate taarifa wangapi wamezingatia ile EMP na kuweka maeneo hayo kama inavyotakiwa kwenye EMP na wangapi hawajafanya. Wale ambao hawajafanya, mnipe orodha lakini muwe tayari mmesha waandikia barua. Nataka tarehe m...

DC Shekimweri aagiza kampeni maalum ya usafi kukabiliana na El Nino

Na. Coletha Charles, NZUGUNI TANROADS, TARURA, DUWASA na Serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma zimetakiwa kuendesha kampeni maalum ya usafi wa mitaro, makalavati na madaraja katika kipindi cha Mwezi Agosti, Septemba na Oktoba, 2026 ili kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua kubwa za El Nino.   Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri katika viwanja vya Dkt. John Malecela Kata ya Nzuguni, wakati wa utekelezaji wa maelekezo ya serikali ya kuchukua hatua za mapema kukabiliana na athari zinazoweza kusababishwa na mvua zitakazonyesha kwa kiwango cha juu ya wastani.   Alhaj Shekimweri alisema kuwa mvua nyingi huleta athari katika makazi ya watu kutokana na kuzibwa kwa mitaro, makalavati na madaraja, hususan kwa taka na michanga.   “TANROADS na TARURA, mnatakiwa kutangulia mkafanye ukaguzi wa hiyo miundombinu ya barabara. Na mimi nitapenda kupewa taarifa ya ukaguzi wenu umebainisha wapi na wapi na kama kun...

Ziara ya DC kukagua ujenzi wa Barabara Dodoma

  Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Alhaj Jabir Shekimweri, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara tatu zinazotekelezwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. •      Barabara Nzuguni – kwa Masista (KM 0.5) kwa kiwango cha lami, pamoja na Barabara ya Nzuguni – Makaburini (KM1.5) kwa kiwango cha changarawe, ikiwa na gharama ya shilingi milioni 694.1 fedha kutoka Road Fund Development. •      Mradi wa uboreshaji wa Barabara ya Mwangaza (KM1.1) kwa kiwango cha lami, kwa gharama ya shilingi Bilioni 1.6. •      Mradi wa uboreshaji wa Barabara ya Mwangaza – Mwambosa (KM 0.7) kwa kiwango cha lami, gharama ya mradi ni shilingi milioni 880.1.

Miundombinu ya elimu kuing’arisha Msembeta S/M

Na. Jesca Kipingu, DODOMA Mradi wa umaliziaji wa ujenzi wa matundu 13 ya vyoo katika Shule ya Msingi Msembeta, umefikia asilimia 90 ya utekelezaji, ambapo kazi mbalimbali za ujenzi na umaliziaji wa miundombinu hiyo zinaendelea kwa kasi kuelekea kukamilika kwake. Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi 38,905,912.75, fedha zinazotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Sambamba na hilo, halmashauri imefanikiwa kukamilisha kwa asilimia 100 mradi wa umaliziaji wa nyumba moja ya mwalimu katika Shule ya Msingi Msembeta. Mradi huo umegharimu jumla ya shilingi 40,100,000, fedha ambazo pia zimetolewa kupitia mapato ya ndani ya halmashauri. Kukamilika kwa miradi hii kunatarajiwa kuleta nafuu kwa walimu na wanafunzi, huku kukiwa na ongezeko la mazingira bora ya ufundishaji na ujifunzaji. Uwekezaji huo unaendelea kuonesha dhamira ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kuimarisha sekta ya elimu kwa kutambua kuwa miundombinu bora ni msingi muhimu wa utoaji wa elim...

Dodoma CC Yatwaa Ubingwa wa Mpira wa Mikono SHIMISEMITA, 2026

Na. Leah Mabalwe, MBEYA   Timu ya Mpira wa Mikono ya Wanaume kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma imetwaa ubingwa wa mashindano ya SHIMISEMITA yanayofanyika jijini Mbeya, baada ya kuicharaza Halmashauri ya Wilaya ya Geita magoli 9-6 katika mchezo wa fainali.   Mchezo huo wa kusisimua ulifanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Samora, ambapo timu zote mbili zilionesha ushindani mkubwa katika kuwania taji hilo.   Akizungumza mara baada ya mchezo huo, Kocha wa Timu ya Mpira wa Mikono ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Baraka Muhamed alisema kuwa mchezo huo ulikuwa mgumu kutokana na timu zote mbili kuwa zilijiandaa vizuri kwa ajili ya kuwania ubingwa. “Mchezo ulikuwa mgumu kwa sababu pande zote mbili zilikuwa zimejipanga vizuri kwa ajili ya kuwania ubingwa huu. Tumejituma sana hadi kufikia hatua hii. Nawashukuru sana wachezaji wote kwa kujituma na kutupa ushindi huu” alisema Muhamed.   Kwa upande wake, Nahodha wa Timu hiyo, Charles Malima alisema kuw...