Posts

Showing posts from June 3, 2026

Msalala DC wajifunza mbinu za ukusanyaji mapato kupitia mfumo wa kanda Dodoma Jiji

Na. Mwandishi Wetu Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imetembelea Ofisi ya utoaji huduma Kanda Namba Moja iliyopo Soko la wazi la Machinga, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ili kujifunza mbinu za ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa kanda ambao umesaidia kuongeza ufanisi wa makusanyo na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Akielezea namna ya utendaji kazi wa kanda hiyo, Nicholaus Mitembo, Meneja wa Kanda Namba Moja, alisema kuwa kanda hiyo inatoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara na kuwahamasisha kulipa mapato kwa hiari na kwa wakati ili kuepuka adhabu na pia kuchangia maendeleo ya eneo lao. Aidha, alisema kanda hiyo inatarajia kukusanya mapato ya shilingi 19,162,421,314.32. Nae, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Rose Manumba, aliishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kukubali na kutoa nafasi ya kujifunza katika halmashauri hiyo. Aidha, aliwakaribisha viongozi na watumishi wa jiji hilo kutembelea Msalala kwa ajili ya kujifunza zaidi kuhusu shughuli kuu za k...

Msalala DC watembelea Jiji la Dodoma kujifunza ukusanyaji Mapato

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Madiwani na Wataalum wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala wamefanya ziara ya mafunzo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujifunza mbinu mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo. Akiwasilisha taarifa ya ukusanyaji na usimamizi wa mapato, Mhasibu wa Mapato wa Jiji la Dodoma, Julius Shinji katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, alisema kuwa katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, halmashauri ilijiwekea lengo la kukusanya jumla ya shilingi 71.675,239,000 kutokana na vyanzo vya ndani. Alisema kuwa hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2026, halmashauri ilikuwa imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi 61,328,048,214.71, sawa na asilimia 85.56 ya lengo la makisio ya mwaka. “Ukusanyaji wa mapato unafanyika kupitia mfumo wa kanda. Halmashauri tumeunda kanda saba za utoaji huduma zenye wataalamu kutoka divisheni na vitengo mbalimbali kupitia ukusanyaji wa moja kwa moja na kwa kudhibiti mianya ya upotevu. Makisio ya mapato kwa Mwaka wa Fedha 2026/202...