Posts

Showing posts from October 15, 2024

Wananchi waliojiorodhesha Mkonze wawe Mabalozi kuhamasisha wengine

Image
  Na. Dennis Gondwe, BWAWANI, MKONZE WANANCHI waliojiorodhesha katika orodha ya wapiga kura wameshauriwa kuwa mabalozi ili kuhamasisha wenzao ambao hawajajiorodhesha kufanya hivyo mapema ili kuepuka foleni siku ya mwisho hatua itakayowawezesha kuchagua viongozi bora. Mkazi wa Mtaa Bwawani, Kata ya Mkonze, Patrick Richard baada ya kujiandikisha Rai hiyo ilitolewa na mkazi wa Mtaa Bwawani, Kata ya Mkonze, Patrick Richard muda mfupi baada ya kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika kituo cha Ofisi ya Afisa Mtendaji Mtaa wa Bwawani mapema leo. Richard alisema “mimi nimetumia muda mfupi sana, chini ya dakika moja kujiandikisha katika daftari la wapiga kura wakati nilijua nitatumia muda mrefu. Kumbe hata wakija watu 10 kwa pamoja watatumia chini ya dakika 10 kujiandikisha. Wito wangu wananchi waje kwa wingi kujiandikisha katika kituo hiki kilichopo kwenye Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Bwawani. Sisi ambao tumeshajiandikisha na kuona uandikishaji ulivyo tuwe mabalozi tu...

Viongozi bora wanachaguliwa na wananchi waliojiorodhesha

Image
Na. Dennis Gondwe, MWAJA, CHAMWINO VIONGOZI bora wa serikali za mitaa wanachaguliwa na wananchi waliojiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili waweze kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Mkazi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Josephine Joseph wakati akijiandikisha katika orodha ya wapiga kura  Kauli hiyo ilitolewa na mkazi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Josephine Joseph alipoongea na mwandishi wa habari hii muda mfupi baada ya kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika kituo cha Shule ya Msingi Chinangali. Joseph alisema kuwa kujiandikisha ni haki yake na haki ya kila mwananchi mwenye sifa za kujiandikisha. “Viongozi bora wa serikali za mitaa wanachaguliwa na wananchi wenyewe. Hivyo, ili uweze kumchagua kiongozi bora, sifa ya kwanza uwe umejiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura katika mtaa wako. Bahati nzuri sifa ni za kawaida sana, kwamba awe na umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea, awe mtanzania mwenye akili timamu zaidi awe ni mkazi wa mtaa ambao u...