Posts

Showing posts from October 10, 2025

Kanda Namba Moja yaendelea kutoa Huduma kwa Mteja

Image
 

Kanda Namba Moja na Huduma kwa Mteja

Image
 

Huduma bora ni msingi wa kazi Kanda Namba Tatu

Image
Na. Mwandishi Wetu, KIZOTA Kanda Namba Tatu yaonesha kiwango bora cha huduma kwa wateja kwa kuendelea kufanya vizuri katika kutoa huduma zinazogusa matarajio ya wananchi wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja. Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Kanda Namba Tatu ya utoaji huduma katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fanuel Lawrence alipokuwa akiongelea Wiki ya Huduma kwa Mteja katika kanda hiyo. Alisema kuwa huduma bora ni wajibu wa kila mtumishi wa umma na njia ya kuj enga imani na uaminifu wa wananchi kwa serikali yao. “Huduma bora ni msingi wa kazi yetu, tunapaswa kuwa na mbinu mpya, kuwa na adabu, na kujitolea ili wananchi wapate huduma stahiki” alisema Lawrence. Aidha, aliwakaribisha wananchi na wafanyabiashara katika ofisi ya Kanda Namba Tatu zilizopo katika pamoja na Ofisi ya Afisa Mtendaji Kata ya Kizota kupata huduma zote muhimu. Aliongeza kuwa ofisi hizo zimesogezwa karibu na wananchi ili kuwapunguzia kero ya kufuata huduma mbali na makazi na shughuli zao. Nae, A...

Kanda Namba Mbili yang'ara kwa huduma bora kwa wateja

Image
Na. Tutindaga Nkwindi DODOMA Kanda Namba Mbili imeendelea kung ’ ara kwa kutoa huduma bora zenye tija kwa wananchi katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja yanayoendelea katika ofisi ya kanda kwa kushirikisha watumishi pamoja na wananchi kutoka maeneo mengi ya kata zinazounda kanda hiyo. Maadhimisho hayo ni ukumbusho wa kuimarisha mawasiliano kati ya watumishi na wananchi, sambamba na kujadili changamoto na mafanikio katika utoaji wa huduma kwa umma.   Meneja wa Kanda Namba Mbili, Abeid Msangi alisema kuwa utoaji wa huduma bora ni wajibu wa kila mtumishi wa umma na njia sahihi ya kujenga uaminifu wa wananchi kwa taasisi za serikali. “ Huduma bora kwa wateja ni moyo wa utendaji. Tunapaswa kuwa wabunifu, wakarimu na kujituma ili kila mwananchi ajisikie kuthaminiwa anapohudumiwa ” alisema Msangi. Kwa upande wake, Afisa Biashara wa Kanda Namba Mbili, Ruth Kingu alisema kuwa Wiki ya Huduma kwa Mteja ni fursa muhimu ya kupokea mrejesho kutoka kwa wananchi na kuboresha zaidi ...

Kanda Namba Mbili yaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi

Image
Na. Tutindaga Nkwindi, NZUGUNI Kanda Namba Mbili inayohudumia kata tano za Nzuguni, Ipagala, Ihumwa, Mtumba na Kikombo imeendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha kila mkazi wa kanda hiyo anapata huduma kwa wakati na kwa kiwango kinachostahili. Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Kanda hiyo, Abeid Msangi alisema kuwa kanda imejipanga vizuri katika kusimamia utoaji wa huduma kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, ubunifu na uwajibikaji. “ Tunaendelea kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa haraka na kwa ubora. Tumeweka mifumo ya ufuatiliaji wa maombi ya wananchi na kuboresha mawasiliano kati ya ofisi na jamii ili kuongeza ufanisi ” alisema Msangi. Aidha, alieleza kuwa maafisa walioko katika kanda hiyo wamekuwa wakipatiwa mafunzo ya mara kwa mara kuhusu utoaji wa huduma kwa wateja na matumizi ya teknolojia katika kushughulikia maombi ya wananchi, hatua ambayo imepunguza changamoto za ucheleweshaji wa huduma. Vilevile, alisisi...

Jiji la Dodoma lajikita kuimarisha Mawasiliano na wananchi Wiki ya Huduma kwa Mteja

Image
Na. Leah Mabalwe,   DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatumia maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja kutathmini mfumo wa utoaji huduma kwa wananchi na kuhamasisha mawasiliano bora ili kuwaweka wananchi karibu zaidi na halmashauri yao. Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Dennis Gondwe akifafanua jambo Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dennis Gondwe, alipokuwa akijibu swali la jinsi halmashauri inavyotumia maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja ofisini kwake. Gondwe alisema kuwa Wiki ya Huduma kwa Mteja ni wiki inayoikumbusha halmashauri kuwa ipo kwa ajili ya utoaji huduma kwa wananchi. “Msingi wa uwepo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni utoaji wa huduma bora na za viwango kwa wananchi. Ni kipindi ambacho tunatafakari hali ya huduma tunayotoa kwa wananchi, ni kipindi ambacho tunatafakari kule tunapolenga kufika katika viwango vya utoaji wa huduma. Menejimenti ya halmashauri inalenga kufika sehemu am...