Na. Mwandishi wetu, DODOMA WANANCHI wametakiwa kuzingatia ulaji bora wa chakula kwa ajili ya kuboresha na kulinda afya kwa kutumia mazao yanayozalishwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili wawe na lishe bora itakayowasaidia kutekeleza majukumu ya kujenga taifa. Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia masuala ya Afya, Prof. Tumaini Nagu alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma. Prof. Nagu aliwasisitiza wananchi kuzingatia ulaji wa chakula bora kwa ajili ya afya bora, akisema kuwa mazao yanayozalishwa katika Jiji la Dodoma ni bora na yanamchango mkubwa katika kuboresha lishe. “Niwapongeze Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri mnayoifanya. Pia niwasisitize wananchi hasa vijana kula chakula bora kama tulivyojionea hapa. Mazao yanayozalishwa ni mazao bora kabisa kwa afya. Hivyo, vijana kama kizazi cha baadae wajitahidi kula ...