Posts

Showing posts from October 9, 2024

Jiji la Dodoma wahamasishwa kujiandikisha orodha ya wapiga kura

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wananchi wamehamasishwa kujitokeza kwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ifikapo Oktoba 11 hadi 20, 2024 kwa lengo la kuchagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Ushauri huo ulitolewa na Diwani wa Viti Maalum Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Asma Karama muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Kamati ya Mipango miji na Mazingira katika Shule ya Sekondari Umonja iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Karama ambae ni Naibu Meya Mstaafu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alitoa rai kwa wana Dodoma na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kushiriki katika kujiorodhesha kwenye daftari la wapiga kura kwa sababu ni muhimu kwa wananchi kutumia haki yao. Alisema kuwa kuwa uchaguzi utawasaidia kupata viongozi bora. “Uchaguzi ni gharama, hivyo serikali hugharamia chaguzi kwa ajili ya kukupa haki wewe mtanzania, ikiwa na maana wanataka uchague kiongozi unayemtaka sio uchaguliwe kiongozi” alise...

Maafisa Waandikishaji Jiji la Dodoma watakiwa kufungua vituo kwa wakati

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Maafisa waandikishaji Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameaswa kuzingatia muda wa kufungua na kufunga vituo vya uandikishaji orodha ya wapiga kura unaotarajiwa kufanyika tarehe 11-20 Oktoba, 2024. Wito huo ulitolewa katika mafunzo kwa maafisa waandikishaji wa Jiji la Dodoma yaliyofanyika katika ukumbi wa Mtumba Complex tarehe 08 Oktoba, 2024 na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga. Akizungumza na maafisa waandikishaji orodha ya wapiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuzingatia muda wa kufungua   na kufunga vituo vya kujiandikisha wapiga kura ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pindi wawapo katika maeneo yao ya kazi. “Vituo vyetu kama mlivyotangaziwa vitafunguliwa saa mbili kamili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili jioni. Sasa isije ikatokea ukaona hakuna watu ukaweka vitabu kwenye begi ukaondoka. Sisi tunapita kukagua kila kituo na bahati nzuri kila kata, kila mtaa kuna mtu anayesimamia huo mtaa. Kwahiyo, kuna...