Posts

Showing posts from March 10, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma atoa angalizo matumizi ya ‘Internet’ Viwandani Sekondari

Image
Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI Walimu watakiwa kudhibiti matumizi mabaya ya ‘internet’ kwa wanafunzi shuleni ili kukabiliana na mabadiliko makubwa ya utandawazi na matumizi ya teknolojia. Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri wakati wa Hafla ya Ugawaji wa Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani. “Rai yangu ni kwamba tujitahidi kuweka ‘internet’ ili kusudi matumizi chanya kabisa ya maabara hiyo iweze kufanyika. Tukishaweka hiyo ‘internet’ tusisahau kuweka udhibiti ili vijana wetu wawe salama na matumizi yasiyo rafiki ya mitandao. Bahati mbaya wapo vijana wanaotumia mitandao kupenyeza agenda husuani mitaala ambayo haifai kwenye elimu yetu, kwahiyo ili kuzuia hayo ni muhimu kuweka vidhibiti na kuwa makini” alisema Alhaj Shekimweri. Nae, Mwalimu wa Shule ya Sekondari Viwandani, Mwl. Dickson Massatu, alieleza kuwa amefurahi Shule ya Sekondari Viwandani kupatiwa vifaa hivyo kwasababu...

Mbunge Mavunde agawa Kompyuta na Printa Shule za Sekondari za Serikali Dodoma

Image
Na. Leah Mabalwe, VIWANDANI Wanafunzi wa shule za sekondari za serikali waaswa kuongeza jitihada katika masomo yao ili kuzidisha ufaulu. Hayo yalisemwa na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde wakati wa hafla ya ugawaji wa komputa na printa katika shule zote za serikali za sekondari jijini Dodoma na uzinduzi wa maabara ya kisasa ya kompyuta ya Shule ya Sekondari Viwandani. “Napenda kuhamasisha wanafunzi wote wa shule za sekondari kuongeza jitihada sana katika masomo yenu. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sasa anawekeza sana katika sekta ya elimu ili wanafunzi wote mpate mazingira mazuri kwa ajili ya kujisomea. Kwa sasa tunahitaji kujenga Jiji la Dodoma katika sekta ya elimu na kazi kubwa bado zinaendelea kufanyika. Nimeamua kufanya ziara hii ya ugawaji wa kompyuta katika shule zote za Dodoma mjini ili kuwaongezea maarifa pamoja na kukua kwa utandawazi kwasababu tunarahisisha upataji wa maarifa kwa ninyi wanafunzi wote. Kompyuta hizi zina ...

Shule ya Sekondari Viwandani yamshukuru Mbunge Mavunde kuboresha miundombinu ya Elimu

Image
Na. Faraja Mbise, VIWANDANI Uongozi wa Shule ya Sekondari Viwandani wamshukuru Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde kwa kuboresha miundombinu ya shule hiyo sambamba na ujenzi wa maabara mpya ya kompyuta na ugawaji wa kompyuta 20, viti 20 na printa moja. Shukrani hizo zilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Viwandani, Mwl. Ester Simchimba, alipokuwa akitoa taarifa ya shule hiyo katika hafla ya ugawaji Kompyuta na Printa kwa shule za sekondari jijini Dodoma, iliyofanyika tarehe 10 Machi, 2025 katika Shule ya Sekondari Viwandani, Kata ya Viwandani, jijini Dodoma. Akisoma risala hiyo, Mwl. Simchimba alimshukuru mgeni rasmi kwa kuwa mdau mkubwa katika kusimamia taaluma na kuboresha miundombinu ya shule hiyo, sambamba na kutoa nafasi ya kipekee ya kuichagua shule hiyo kuwa sehemu maalum kwa kufanyia tukio hilo la kihistoria katika shule hiyo. “Tunashukuru kwa kuchagua shule yetu kuwa mahali pa kufanyia hafla hii fupi na tukio la kihistoria katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ikiwaki...