Posts

Showing posts from March 25, 2025

Mradi wa Maji ya Mvua uliofadhiliwa na TASAF wasaidia wanafunzi Shule ya Msingi Ipala

Image
Na. Emanuel Charles, IPALA   Mwenyekiti wa Kamati ya TASAF Taifa, Peter Ilomo ameupongeza uongozi wa Kata ya Ipala kwa kuendelea kutunza miradi iliyofadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ukiwemo mradi wa ukusanyaji maji ya mvua unaopatikana katika Shule ya Sekondari Ipala wenye lengo la kuondoa adha ya upatikanaji wa maji kwa wanafunzi shuleni hapo.   Akizungumza katika ziara ya kukagua miradi iliyotekelezwa na TASAF, Ilomo alisema kuwa lengo la kwenda kukagua mradi huo ni kuangalia kama unafanya kazi na kusaidia wanafunzi kama ilivyokusudiwa. ā€œTunashukuru mradi ulianza 2022 na kumalizika 2023, kwakuwa tayari mradi umeshakamilika na jamii inayozunguka mradi huu kwa maana ya wanafunzi na waalimu wananufaika tunasema asante sana. Lengo lakuja hapa ni kukagua kama mradi unafanya kazi kwasababu mara nyingi miradi unaweza kukamilika lakini usifanye kazi, nipongeze uongozi wa hapa Ipala, ninyi mmekuwa wa tofautiā€ alisema Ilomo.   Pia aliongeza kwa kusema ...

Wananchi Matumbulu kufurahia ujenzi ofisi mpya ya Kata

Image
Na. Nancy Kivuyo, MATUMBULU SERIKALI ya awamu ya sita inalenga kuboresha mazingira bora ya kufanyia kazi kwa wafanyakazi wa serikali ili waweze kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kujenga na kuboresha Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Matumbulu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Matumbulu, Zubery Mbawala alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari waliofanya ziara ya kutembelea miradi iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Matumbulu, jijini Dodoma.   Mbawala alisema kuwa ujenzi wa Ofisi ya Afisa Mtendaji wa Kata ya Matumbulu ulianza kwa michango ya nguvu za wananchi. ā€œWananchi walijitolea eneo na wakaanza ujenzi kwa nguvu zao, baadae serikali ndio ikawapokea, kuendeleza ujenzi huo kwa kutoa kiasi cha shilingi 67,000,000 ili kuhakikisha ujenzi huo unakamilika na wananchi wanapata huduma bora. Hata sasa ofisi hii inatumika japo ipo katika hatua za mwisho kukamilikaā€ alisema Mbawala...

Shule ya kwanza ya Sekondari yajengwa Matumbulu tangu Uhuru

Image
Na. Nancy Kivuyo, MATUMBULU Diwani wa Kata ya Matumbulu, Emmanuel Chibago aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu katika sekta ya elimu katani hapo. Diwani wa Kata ya Matumbulu, Emmanuel Chibago, akitoa shukrani kwa rais Alitoa shukrani hizo wakati alipokuwa mwenyeji wa waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali kuanzia mwaka 2020 hadi 2025 katika Kata ya Matumbulu.   Chibago alisema kuwa ni historia kwa Kata ya Matumbulu kuwa na shule ya sekondari na kusema kuwa haijawahi kutokea tangu kupatikana kwa uhuru. ā€œKiukweli, nampongeza sana Rais wetu pamoja na Mbunge Mavunde, wamehakikisha wananchi tunaoishi hadi pembezoni mwa mji tunapata shule ili watoto wetu wapate elimu nzuri. Ukitazama ndugu mwandishi, haya majengo ni ya kisasa kabisa, wanafunzi watasoma katika mazingira mazuri na italeta chachu ya ufaulu kwasababu kule msingi walipo sas...

Rais Samia aboresha huduma ya Maji Matumbulu

Image
Na. Emanuel Charles, MATUMBULU   DIWANI wa Kata ya Matumbulu, Emmanuel Chibago ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya sekta ya afya, elimu, ujenzi wa ofisi ya kata pamoja na mradi wa maji ambao mpaka sasa serikali imefanikiwa kujenga visima 12 vinavyotoa huduma ya maji kwa wananchi wa kata hiyo.   Akiongelea mafanikio ya serikali katika kipindi cha miaka minne kwa waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kuanzia mwaka 2021 hadi sasa katika Kata ya Matumbulu, Diwani Chibago alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kupeleka miradi ya maendeleo katani hapo. Alisema kuwa serikali imechimba visima 12 vya maji ukilinganisha na awali kilikuwepo kisima kimoja tu kikihudumia kata nzima. ā€œNipende kuipongeza serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwasababu mpaka sasa katika Kata ya Matumbulu wananchi hawahangaiki na maji tena tofauti na hapo mwanzo palikuwa na kisima kimoja ch...