Posts

Showing posts from January 27, 2025

Waganga Wafawidhi wa Jiji la Dodoma wapatiwa mafunzo ya Mfumo wa NeST

Na. Halima Majidi, DODOMA Waganga wafawidhi kaitka Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamewezeshwa mafunzo ya ununuzi kwa njia ya mfumo serikalini ‘National e- Procurement System of Tanzania’ (NeST) yatakayoongeza ufanisi na kurahisisha utendaji wa kazi pamoja na kupunguza hoja za ukaguzi kwa sababu kila kitu kitakuwa kipo wazi. Mafunzo hayo yalitolewa na Kitengo cha Manunuzi na Ugavi cha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, kwa lengo la kuongeza ufanisi, kupunguza gharama pamoja na kuokoa muda, ambayo yalifanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Umonga. Mwezeshaji wa Mafunzo hayo, Josephat Nyumayo, alieleza kuwa, mafunzo hayo yalikuwa yanahusu matumizi ya mfumo wa ‘NeST’ katika ngazi ya kata kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Mwaka 2023 na Kanuni zake za Mwaka 2024, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali kuwa manunuzi yote yafanyike kwa mfumo huo. Aidha, Nyumayo alisema kuwa, mafunzo hayo ni ya awamu ya pili kwa waganga wafawidhi ambapo mafunzo ya awali yalikuwa yanahusu matumi...

Elimu Sekondari Jiji yawalaza chali Maafisa Watendaji Mchezo wa Pete

Image
Na. Halima Majidi, DODOMA Katika mchezo uliovuta hisia za mashabiki wengi, Timu ya Mchezo wa Pete ya Elimu Sekondari ya Jiji la Dodoma imeibuka kidedea kwa kuishinda Timu ya Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa Jiji la Dodoma goli 3-2. Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma ulidhihirisha ushindani mkali kati ya timu hizo mbili. Mchezo ulianza kwa kasi huku wachezaji wa Elimu Sekondari wakionesha umahiri wa hali ya juu katika kurusha mpira kwa haraka na ukabaji imara. Katika robo ya kwanza, timu hiyo iliongoza kwa alama 2 dhidi ya 0 za Maafisa Watendaji.   Kocha wa Timu ya Elimu Sekondari, Mwl. Zainabu Abdallah, alisema amefanya yake katika kuhakikisha wanachukua ushindi japokuwa mvua imekuwa kikwazo, na aliwapongeza vijana wake kwa kujituma uwanjani na kutumia mbinu walizofanyia mazoezi, na pia alisisitiza wachezaji wawe na tabia ya kufanya mazoezi sio tu mpaka wakti wa michezo au bonanza bali iwe ni tabia endelevu. “ Ushindi huu ni matokeo ya nidhamu, maz...

Elimu Kombaini FC Yailaza na Viatu Sheria Ndogo FC

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Timu ya Mpira wa Miguu ya Elimu Kombaini imeishushia kipigo cha mbwa mwizi Timu ya Mpira wa Miguu ya Sheria ndogo FC baada ya kuichabanga mabao 3-1 katika mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma ikiwa ni muendelezo wa michezo mbalimbali katika tamasha la kuukaribisha Mwaka 2025 la CCD Watumishi Bonanza lililoandaliwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma. Baada ya mchezo kutamatika Nahodha wa timu ya Elimu Kombaini, Given Alestides, alisema “ tumefanikiwa kupata matokeo na tukiwa kama watu wa elimu tumewafundisha wanasheria jinsi ya kucheza mpira wa miguu na wameelewa, lakini yote kwa yote tumefurahi kushiriki bonanza hili na tumekutana wa watu wengi na tumejifunza mambo mengi sana, tunampongeza sana Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa ubunifu huu alioufanya ”. Nae Nahodha wa Timu ya Sheria ndogo, Salumu Bwenda akatoa sababu zilizowafanya wapoteze mchezo huo kwa idadi kubwa ya mabao. “ Mchezo umeisha na tumepoteza kwa bao 3-1 ni matokeo mabaya lakini sab...

Mtakwimu Mdoya mbabe Mchezo wa Drafti

Image
Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Mtakwimu wa Jiji la Dodoma, William Mdoya ameibuka mshindi katika Mchezo wa Drafti baada ya kumfunga Afisa Michezo, Peter Ititi kwa jumla ya mabao 2-1 ambapo mchezo huo ulilazimika kwenda kwenye muda wa ziada baada ya muda wa kawaida kufungana bao 1-1. Baada ya ushindi huo alisema “ nafurahia ushindi kwa sababu ndio kitu nilichokuwa nakitarajia katika bonanza hili, mchezo ulikuwa mzuri, wachezaji wote niliokutana nao walikuwa wazuri na walionesha ushindani ndiyo maana katika mchezo wa fainali tulienda hadi muda wa ziada ” alisema Mdoya. Nae, Mwalimu Stephen Sebastian, ambaye ni mmoja wa washiriki wa mchezo wa Drafti amekiri kushindwa, hii ni kutokana na ubora wa mpinzani wake. “ Mpinzani wangu alikuwa ni mzuri na anaonekana ni mzoefu katika kucheza drafti na katika mchezo ninakiri kwamba, kuna kushindwa na kushinda na nakubali mpinzani wangu amenizidi mbinu na ujanja katika mchezo huu ” alisema Sebastian. Kwa upande wake Mwamuzi wa Mchezo wa Drafti,...

Ofisi ya Rais Ikulu haishikiki kuvuta Kamba

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Timu ya Ofisi ya Rais Ikulu kuvuta Kamba (wanaume) imeibuka na ushindi wa alama 2-0 dhidi ya Timu ya Ofisi ya Rais Jiji Dodoma kuvuta Kamba (wanaume) katika upande wa wanawake Timu ya Ofisi ya Rais Ikulu ikiibuka na ushindi wa alama 2-0 dhidi Timu ya Ofisi ya Rais Jiji Dodoma katika mchezo huo. Mchezo huo ulifanyika ndani ya Uwanja wa Jamhuri katika Bonanza la Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma lililohusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, michezo ya jadi na tamasha la sanaa. Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa Jiji la Dodoma, Patrick Moshi, aliwataka washiriki wa michezo mbalimbali kujiamini zaidi wawapo uwanjani ikiwa ni njia kufanikiwa na kupata ushindi katika michezo yao. “ Siri ni kufanya mazoezi mapema na wakati wa mchezo ni kujiamini zaidi na hiyo ndio siri ya mafanikio ” alisema Moshi. Mwamuzi wa mchezo wa kuvuta kamba, Idrisa Shabani aliwaomba washiriki wa michezo mbalimbali kuwa na t...

Kilimo yaigaragaza Ardhi, Bonanza la Watumishi, 2025

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Timu ya Mpira wa Miguu ya Watumishi wa Divisheni ya Kilimo Mjini, Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeibuka kidedea baada ya kushinda penati 6-5 dhidi ya Timu ya Mpira wa Miguu ya Watumishi wa Divisheni ya Uendelezaji Makao Makuu. Penati hizo zilipigwa baada ya kutoshana nguvu katika muda wa kawaida ndipo ikaamuliwa kupigwa mikwaju ya penati na Kilimo kuibuka wababe. Mchezo huo ulivurumishwa katika Kiwanja cha Jamhuri Dodoma kwenye Bonanza la kuukaribisha Mwaka 2025 lililoandaliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Baada ya mchezo kutamatika Nahodha wa Timu ya Kilimo FC, Michael Lukumai alisema “toka mchezo unaanza sisi tulikua bora kuliko wao japo walianza kwa kututangulia mabao yote lakini sisi tukawa bora kuliko wao, ndiyo maana tukafanikiwa kurudisha mabao yote na kwenye mikwaju ya penati tukaibuka kidedea, lakini yote kwa yote watumishi wamepata burudani na imekuwa siku ya kihistoria kwetu sote”. Nae, Nahodha wa Timu ya Ardhi FC, Godwin Maselo akaelezea...

Watumishi Waaswa Mshikamano

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Watumishi mbalimbali wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya kazi kwa mshikamano katika kutoa huduma zao kwa jamii ili kuweza kuiinua halmashari izidi kupanda katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Hayo yalisemwa na Diwani wa Kata ya Mtumba, Edward Maboje, alipokuwa akitoa wito katika Bonanza la Watumishi lililofanyika tarehe 25 Januari, 2025 katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. “ Mshikamano uliooneshwa leo uendelee hata katika kutoa huduma kwa jamii kwa ngazi zote. Hili jambo la leo, mkurugenzi na timu yake wameonesha jambo la kutujali watu wa ngazi zote. Kwahiyo, na mimi ninawaomba sasa, watumishi na sisi madiwani tufanye kazi kwa mshikamano na kwa ushirikiano mkubwa ili tuiinue halmshauri yetu izidi kupanda. Mimi nimesema hili ni jambo jipya kwangu na mimi ni mtu mzima, ni jambo jipya. Pia, Dodoma hapa ni nyumbani, napafahamu vizuri na wakurugenzi wanapita wengi lakini hiki kitu kimenigusa na ninawaomba watumishi wa Halmashauri ya Ji...

Watumishi Bonanza lafana Jiji la Dodoma

Na. Faraja Mbise, DODOMA Maelfu ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wajitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Jamhuri kushiriki Bonanza la kuaga na kukaribisha mwaka mpya 2025. Akizungumza wakati wa Bonanza hilo, Diwani wa Kata ya Mtumba, Edward Maboje, alisema kuwa, katika utumishi wake wa miaka kumi hajawahi kuona bonanza la namna hiyo kuwahi tokea na alitumia nafasi hiyo kumshukuru Mkurugenzi wa Jiji kwa kuwakutanisha watumishi wote kwa lengo la kuimarisha mahusiano bora katika utendaji kazi. “ Mimi nina mwaka wa 10 katika udiwani, toka nimekuwa Diwani halijawahi kutokea bonanza kama hili. Nadhani niseme hili bila kuficha, kiongozi wa halmashauri kwa maana ya mkurugenzi, ana upeo mkubwa sana kwa watumishi wake ” alisema Maboje. Kuhusu masuala ya mahusiano mema katika utendaji na uboreshaji wa kazi, alisema, kukutanishwa kwa watumishi hao kunajenga msingi bora wa maelewano na mshikamano. Maboje alisema “ bonanza hili linaonesha namna ambavyo Mkurugenzi ana mahusiano mazur...