Posts

Showing posts from September 29, 2024

Maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa kutoa elimu kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha Mbwa

Image
Na. Asteria Frank, DODOMA   Maadhimisho ya siku ya kichaa cha mbwa duniani yanalenga kuelimisha jamii juu ya kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa pamoja na kutowa chanjo kwa paka na mbwa ili kuwakinga na ugonjwa huo. Maadhimisho hayo yamefanyika katika ofisi za kituo za huduma za mifugo kanda ya kati Dodoma mjini ambapo wamefahamisha kuhusu kichaa cha Mbwa Pamoja na kutoa chanjo, dawa ya kuzuia viroboto na dawa za Minyoo kwa Mbwa na Paka. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hussein Nyenye katika maadhimishi ya siku ya kichaa cha mbwa duniani yaliyofanyika katika Kituo cha Huduma za Mifugo Kanda ya Kati, kilichopo jijini Dodoma. Nyenye alisema kuwa ni muhimu kwa wafugaji wa mbwa na paka kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kuweza kuwapatia mbwa na paka chanjo kwa wakati sahihi kuzuia magojwa mbalimbali kwa wanyama hao na wafugaji wenyewe. Alisema kuwa shughuli ya kudhibiti kichaa cha mbwa haiwezakani kufanyika na watu wa mifugo...

Uboreshaji daftari la wapiga kura chini ya dakika 5

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA   WANANCHI katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kufika katika vituo vya kuandikishia wapiga kura ili kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura mapema kwa sababu zoezi linafanyika chini ya dakika tano. Faraja Mbise baada ya kujiandikisha Ushauri huo ulitolewa na Faraja Mbise, mkazi wa Mtaa wa Chang’ombe, Kata ya Ihumwa, Halmashauri ya Jiji la Dodoma alipofanya mahojiano maalum baada ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura katika Kituo cha Shule ya Msingi Msuguri. Mbise alisema “wito wangu kwa wananchi ambao bado hawajafika katika vituo vyao vya kujiandikisha, wafike mapema kwa sababu zaidi ya siku ya leo zitakuwa zimebaki siku mbili tu. Wajitokeze kwa wingi kujiandikisha kwa sababu zoezi linaenda vizuri sana na kwa haraka. Ni zoezi ambalo halichukui hata zaidi ya dakika tano”. Aidha, akiongelea utendaji wa maafisa uandikishaji, alisema kuwa wanafanya kazi vizuri. “Maafisa uandikish...

Vijana wahamasishwa kujiandikisha Daftari la Kudumu la Wapiga kura

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MAKULU VIJANA wameshauriwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili waweze kushiriki zoezi la Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Magdalena Samwel, mkazi wa Mtaa wa Mwangaza Kata ya Dodoma Makulu Ushauri huo ulitolewa na Magdalena Samwel, mkazi wa Mtaa wa Mwangaza Kata ya Dodoma Makulu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma muda mfupi baada ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura kwenye kituo kilichopo Shule ya Sekondari Kisasa leo asubuhi. Samwel alisema “leo nimewahi hapa kituoni kwa ajili ya kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ili niwahi kazini. Nimejiandikisha nikiwa mtu wa pili, ulinitangulia wewe ndugu mwandishi. Nimekuja ili nipate uhalali kwa kushiriki uchanguzi mkuu ujao kama mtanzania”. Aidha, alitoa wito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura. “Napenda kuwashauri vijana wajitokeze kwa w...