Posts

Showing posts from November 14, 2023

Waziri Mkuu Majaliwa Avutiwa Na Mchango Wa NBC Kuchochea Kasi Ya Kilimo, Biashara Na Michezo

Image
   Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameonyesha kuvutiwa na mchango unaoendelea kutolewa na benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika kukuza sekta mbalimbali nchini ikiwemo kilimo, biashara na michezo kupitia huduma na ufadhili wa benki hiyo kwenye maeneo hayo. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (Kulia) akizungumza na baadhi ya maofisa wa benki ya NBC akiwemo Meneja wa NBC tawi la Lindi Bw. Iovin Mapunda (Kushoto) na Meneja Mahusiano wa beniki hiyo Bi Brendansia Kileo (Katikati) wakati alipotembelea banda la benki hiyo lililopo kwenye viunga vya ukumbi wa Mkutano Mkuu wa saba wa mwaka wa Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Mkoani Lindi. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi Zainabu Telack. Benki ya NBC ni moja ya wadhamini muhimu wa Mkutano huo wa siku mbili Waziri Mkuu Majaliwa alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la benki hiyo lililopo kwenye viunga vya ukumbi wa Mkutano Mkuu wa saba wa mwaka wa Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Mkoani Lindi. Benki ya NBC ni moj...

Mkurugenzi Mkuu Wa VETA Afanya Ziara Ofisi Za VETA Kanda Ya Kati Na Chuo Cha VETA Dodoma

Image
    MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Prosper Mgaya amefanya ziara katika Ofisi za VETA Kanda ya Kati na Chuo cha VETA Dodoma ambapo ametembelea karakana kujionea shughuli za mafunzo na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Kanda na Chuo.   Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Prosper Mgaya akiwa katika Chuo cha VETA Dodoma na Ofisi ya   VETA  Kanda ya Kati Akizungumza wakati wa ziara hiyo leo tarehe 13 Novemba, 2023, Dkt. Mgaya ameainisha mikakati mbalimbali ya kuboresha utoaji mafunzo ya ufundi stadi nchini ili kuwanufaisha wananchi wengi zaidi na kuwawezesha kuendesha shughuli za kiuchumi kwa ufanisi.   Mikakati hiyo ni pamoja na kuongeza ubunifu kwenye kuandaa kozi za muda mfupi zinazojibu mahitaji halisi ya jamii, kuboresha vifaa vya utoaji mafunzo vinavyokidhi ukuaji wa teknolojia na kuhakikisha ubiasharishaji wa vifaa vya kiubunifu vinavyozalishwa kw...

WAZIRI JAFO AWATAKA WAWEKEZAJI WA BIASHARA YA KABONI KUWA WAWAZI

Image
   Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Selemani Jafo amewataka wawekezaji wa Biashara ya Kaboni nchini kuwa wawazi katika biashara hiyo. Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Selemani Jafo na viongozi mbalimbali wakionesha mfano wa hundi yenye thamani ya sh. Bilioni 4.7 aliyoikabidhi kwa ajili ya wakazi wa Wilaya za Kiteto na Mbulu ambazo zimenufaika na Biashara ya Kaboni Ametoa maelekezo hayo wakati wa hafla ya makabidhiano ya hundi ya malipo ya sh. bilioni 47 kwa wakazi wa Wilaya za Kiteto na Mbulu ambazo zimenufaika na mradi huo mkoani Manyara leo Novemba 14, 2023. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Jafo amewaelekeza wawekezaji kuwa na vyeti vinavyoonesha mahali walipouza bidhaa zao ili kuwa wawazi kwa mujibu wa kanuni ya 4 ya Sheria ya Mazingira inayowataka kuwa na uwazi katika biashara zao. Kwa muktadha huo amewataka kuwa wawazi zaidi na mchanganuo unaoonesha mwanakijiji na mwekezaji wananufaikaje na Biashara ya...

Kamati Ya Bunge Ya Mambo Ya Nje, Ulinzi Na Usalama Imeridhika Na Uendeshaji Na Uendelezaji Wa Kiwanda Cha Maji Cha Uhuru Peak

Image
  KAMATI ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama imeridhika na uendeshaji na uendelezaji wa Kiwanda cha maji cha Uhuru Peak kinachoendeshwa na Suma JKT baada ya kuongeza uzalishaji wa maji. Hivyo, imeyataka mashirika ya umma, Wizara na taasisi za serikali zinunue maji ya Uhuru Peak ili kuendeleza ukuaji wa kiwanda hicho.   Akizungumza leo walipotembelea kiwanda hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge la Tanzania Vita Kawawa amesema maagizo ya serikali yalielekeza taasisi za serikali wanapoandaa shughuli mbalimbali wanunue maji yanayozalishwa na Suma JKT.   Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge la Tanzania Vita Kawawa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea Kiwanda cha Maji cha Uhuru Peak kilichopo JKT Mgulani jijini Dar es Salaam leo Amesema hapo awali kiwanda hicho kilikuwa kinazalisha lita 250 kwa saa na baada ya kufunga mitambo mipya yenye uwezo mkubwa wanazalisha lita 10...

VYOMBO VYA HABARI VISIIACHIE DCEA PEKE YAKE VITA DAWA ZA KULEVYA- DK. RIOBA

Image
Na Said Mwishehe,Michuzi TV WAANDISHI wa habari nchini wameshauriwa kushirikiana na Mamlaka ya Kupambana na Kudhibiti Dawa za Kulevya (DCEA) katika mapambano ya dawa hizo, kwani vita hiyo ni ngumu hivyo DCEA haitakiwi kuachwa peke yake. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Habari Tanzania( TBC) Dk.Ayub Rioba akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari wakati wa semina iliyoandaliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya( DCEA) kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali yanayohusu vita dhidi ya dawa za kulevya Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayub Rioba, wakati akitoa mada kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kupambana na dawa za kulevya kwenye semina ya wahariri wa vyombo vya habari iliyoandaliwa na DCEA. Amesema vyombo vya habari vina wajibu wa kushirikiana na DCEA katika mapambano ya dawa za kulevya ikiwemo vile vya maudhui (mitandaoni) kwani mchango mkubwa kwenye vita hiyo. Dk. Rioba, amesema tafiti zinaonesha biashara...

WATUHUMIWA 188 WAKAMATWA, WAWILI WAKUTWA WAKISAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA KILO 298

Image
  Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi. Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 188 kwa makosa mbalimbali ikiwemo ya wizi na usafirishaji wa dawa za kulevya ambapo kati yao, wawili wamekamatwa na bunda 542 za madawa ya kulevya yadhaniwayo kuwa ni mirungi yenye uzito wa kilo 298. Akitoa taarifa hiyo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Salvas Makweli leo Novemba 14, 2023 amesema Jeshi hilo lilifanya operesheni maalumu kuanzia Oktoba 13, 2023 hadi Novemba 13, 2023 kwa lengo la kuwakamata watuhumiwa wanaojihusisha na matukio ya uhalifu na kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao. ACP Makweli amebainisha kuwa Novemba 12, 2023 muda wa saa 03:00 asubuhi huko katika maeneo ya Philips katika Halmashauri ya Jiji la Arusha walifanikiwa kumkamata Gilbert Joseph (33) mkazi wa Sinoni Jijini Arusha na Peter Waweru (33) mkazi wa Nchi Jirani wakiwa wanasafirisha madawa ya kulevya yadhaniwayo kuwa ni Mirungi Bunda 542 yenye uzito wa k...

HALI YA UPATIKANAJI WA CHAKULA NCHINI YASAIDIA KUPUNGUZA UMASIKINI

Image
Na. Josephine Majura na Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam Tanzania imekuwa kwenye kiwango kizuri cha upatikanaji wa chakula kutokana na kuwepo kwa takwimu sahihi za hali ya Maisha katika kaya, hali iliyopolekea kiwango cha umasikini wa chakula kushuka nchini. Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akifungua Mkutano wa Maadhimisho ya Miaka 15 ya Mradi wa Utafiti wa Kupima Hali ya Maisha zinazojumuisha Tafiti za Kilimo Katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, uliofanyika katika Hoteli ya Delta jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa siku mbili umehudhuriwa na watalamu wa uchumi, sera na watafiti kutoka nchi mbalimbali za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo matokeo ya baadhi ya tafiti zilizofanyika chini ya mradi huo zinawasilishwa Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), wakati akifungua Mkutano wa Maadhimisho ya Miaka 15 ya Mradi wa Utafiti wa Kupima Hali ya Maisha zinazojumuisha Tafiti za Kilimo Katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Saha...