Waziri Mkuu Majaliwa Avutiwa Na Mchango Wa NBC Kuchochea Kasi Ya Kilimo, Biashara Na Michezo

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameonyesha kuvutiwa na mchango unaoendelea kutolewa na benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika kukuza sekta mbalimbali nchini ikiwemo kilimo, biashara na michezo kupitia huduma na ufadhili wa benki hiyo kwenye maeneo hayo. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (Kulia) akizungumza na baadhi ya maofisa wa benki ya NBC akiwemo Meneja wa NBC tawi la Lindi Bw. Iovin Mapunda (Kushoto) na Meneja Mahusiano wa beniki hiyo Bi Brendansia Kileo (Katikati) wakati alipotembelea banda la benki hiyo lililopo kwenye viunga vya ukumbi wa Mkutano Mkuu wa saba wa mwaka wa Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Mkoani Lindi. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi Zainabu Telack. Benki ya NBC ni moja ya wadhamini muhimu wa Mkutano huo wa siku mbili Waziri Mkuu Majaliwa alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la benki hiyo lililopo kwenye viunga vya ukumbi wa Mkutano Mkuu wa saba wa mwaka wa Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Mkoani Lindi. Benki ya NBC ni moj...