Posts

Showing posts from August 8, 2025

Mkurugenzi Mkuu wa TCAA Atembelea Maonesho ya Nanenane 2025 Jijini Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Salim Msangi, atembelea banda la TCAA pamoja na mabanda mengine kadhaa katika Maonesho ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Ziara hii ililenga kuonyesha huduma zinazotolewa na TCAA na kuhamasisha umma kuhusu masuala ya usafiri wa anga. Katika ziara hiyo, Msangi alionesha kuridhishwa na namna TCAA inavyotoa huduma na elimu kwa wananchi, hasa kuhusu usalama wa anga, matumizi salama ya ndege zisizo na rubani (ndege nyuki), na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya usafiri wa anga. Alieleza kuwa huduma zinazotolewa na TCAA zinachangia pakubwa katika kuimarisha usalama na maendeleo ya sekta hiyo. Vilevile, alifurahishwa na ushirikiano wa watumishi wa TCAA katika kuelimisha umma, akiwapongeza kwa kujituma na kuendelea kutoa taarifa muhimu kwa wananchi kuhusu masuala ya usafiri wa anga. Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na wadau wengine katik...

Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu yafungua Masoko ya Nje kwa Wafanyabiashara nchini

Image
Na. Calvin Gwabara, DODOMA Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) imewezesha Tanzania kuondolewa vikwazo vya kiubora iliyowekewa kwenye masoko mbalimbali duniani na hivyo kusaidia wakulima wa Tanzania kunufaika na uuzaji wa mazao nje ya nchi. Hayo yalibainishwa na mtaalamu wa afya ya mimea kutoka TPHPA, Dorah Amur wakati akimueleza Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk alipotembela banda la TPHPA kwenye maonesho ya wakulima Nanenane kitaifa Jijini Dodoma kuhusu mafanikio na jitihada zinazofanywa na Taasisi hiyo katika kuhakikisha ubora wa mazao na kufungua masoko. “Wakulima wa wafanya biashara wa Tanzania wamekuwa wakiuza bidhaa zao kwenye masoko mbalimbali ya kimataifa duniani lakini kuna baadhi ya masoko yalizuia Tanzania kuingiza bidhaa zetu kutokana na sababu mbalimbali za kiubora lakini TPHPA ikaalifanyia kazi haraka kwa kufanya uchunguzi wa kina na kuwasilisha kwenye mamlaka za masoko hayo na kufanikiwa kuondolewa kwa zuio hilo ...

Manaibu Makatibu Wakuu OR TAMISEMI Watembelea Banda la TARURA

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Manaibu Makatibu Wakuu wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI wakiongozwa na Mhandisi Rogatus Mativila Naibu Katibu Mkuu (Miundombinu), Sospeter Mtwale - Naibu Katibu Mkuu (TAMISEMI) na Prof. Tumaini Nagu - Naibu Katibu Mkuu (Afya) wametembea Banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) katika kilele cha Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima NaneNane katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.   Makatibu Wakuu hao walipatiwa maelezo mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa TARURA wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, Catherine Sungura kuhusu majukumu, utekelezaji wa miradi mbalimbali pamoja na mipango ya TARURA inayohusu uboreshaji na ujenzi wa miundombinu ya barabara nchini.    Akizungumza kwa niaba ya wenzake Naibu Katibu Mkuu, Sospeter Mtwale amewapongeza TARURA kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kufungua barabara hususan maeneo ya wakulima, wavuvi na wafugaji na hivyo kuwarahisishia kusafirisha mazao yao.   Pia ...

Pinda ataka matokeo ya Utafiti yazingatiwe kueleza faidia za Kisanyansi katika bidhaa za Kilimo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda ametaka Utaalamu wa Kisanyansi uzingatiwe katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya Kilimo ikiwa ni pamoja na kuzingatia ufafanuzi wa Kisanyansi katika chapa za bidhaa mbalimbali za Kilimo zilizoongezewa thamani ili kuonesha tija inayopatikana kwa mtumiaji wa bidhaa hizo. Mhe. Pinda alisema hayo alipotembelea Banda la Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kwenye Maonesho ya kimataifa ya Kilimo maarufu kama Nanenane yanayoendelea viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma ambapo TARI inashiriki ikiwa na Teknolojia mbalimbali za Kilimo. Akitolea mfano wa Korosho iliyoongezewa thamani na TARI Mhe. Pinda alieleza kufuraishwa na ufafanuzi wa kitaalamu uliopo katika mfuko wa Korosho hizo unaotoa maelezo ya Kisanyansi kumtosheleza mtumiaji kutambua tija anayopata kutokana na matumizi ya bidhaa hiyo zaidi ya kuishia kusema ni tamu yenye ladha nzuri kitu ambacho amesema kinanyima fursa zai...

Bustani inayohamishika mbombozi kwa wenye maeneo haba ya Kilimo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mafunzo yanayotolewa katika vyuo vya VETA yanalenga kuleta utatuzi wa changamoto mbalimbali katika jamii. Watu wengi wanaoishi katika maeneo ya mijini wamekuwa na maeneo finyu kwa ajili ya kilimo, hali hiyo ikampelekea Mwl. Gema Ngoo wa Chuo cha VETA Kihonda, kubuni bustani ya mbogamboga inayohamishika. Akizungumza katika Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo (Nanenane), yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma Mwl. Ngoo ambaye anafundisha Fani ya Ufundi wa Zana za Kilimo alisema ubunifu huo wa bustani inayohamishika ni mahkususi kwa wale watu wanaoishi katika nyumba za kupanga, nyumba zenye maeneo finyu au zilizosakafiwa kote, hivyo kupelekea kukosa sehemu ya kupanda mbogamboga. “Ubunifu huu utawasaidia wengi wenye maeneo finyu kwaajili ya kupanda mbogamboga, tunashauri watu walime kilimo cha aina hii kwani hakiharibu mazingira lakinini pia kilimo hiki utatumia mbolea ya asili ambayo ni salama kwa afya za binadamu” alisema Mwl. Ngoo. Mwalimu G...

VETA yapongezwa kutoa mafunzo kwa wanawake na Samia

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imepongezwa kwa kuendelea kutoa  mafunzo ya ufundi stadi  kupitia Mpango wa mafunzo unaotekelezwa na  Taasisi ya Wanawake na Samia .   Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa  Dodoma , Rosemary Senyamule  ambae ndie muasisi wa Taasisi hiyo, alipotembelea  banda la VETA  lililopo katika viwanja vya Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo (Nanenane),  Nzuguni , jijini Dodoma na kuongea na wahitimu wa mafunzo hayo wanaoonesha bidhaa mbalimbali walizotengeneza baada ya kupata mafunzo kutika vyuo vya VETA.   “Tunafahamu fika kwamba Mhe. Rais wa Jamhuri wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania , Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akihimiza utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi kwa makundi maalum wakiwepo wanawake. Naipongeza VETA kwa kuendelea kuunga mkono juhudi hizo kwa kuwa tunaona matokeo yake kupitia bidhaa na bunifu mbalimbali zinazofanywa na wanawake hapa Dodoma n...

Mtaji Benki ya TADB wafikia Bil. 442

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwekeza katika uwezeshaji wakulima kwa kuwapatia mikopo ya Pembejeo. Akitoa maelezo kwa Mhe. Rais Samia kuhusu utendaji wa Benki hiyo leo Agosti 8,2025 wakati wa maadhimisho ya kilele cha Nanenane kitaifa, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Frank Nyabundege alisema kuwa mtaji wa Benki hiyo umekuwa kutoka shilingi bilioni 60 hadi bilioni 442. “Benki yetu itaendelea kudhamini maonesho ya NnNe Nane kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kwa sababu imeiwezesha kuwa na mtaji mkubwa” alisisitiza Nyabundege. Mgeni rasmi katika maonesho ya Nanenane Kitaifa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.  

Waziri Mkuu Mstaafu, Pinda atembelea NSSF, Maonesho ya Nanenane Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda ametembelea Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Ofisi hiyo pamoja na Taasisi zake ikiwemo NSSF. Maonesho ya Nanenane 2025 Kitaifa yanaendelea katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma ambapo kilele chake ni tarehe 8 Agosti 2025.   Akitoa maelezo mbele ya Mhe. Pinda, Meneja wa NSSF Mkoa wa Dodoma, Yahya Mudhihir, alieleza namna ambavyo NSSF imeboresha utoaji wa huduma kwa kutumia mifumo ya kidijitali, hatua inayolenga kuongeza ufanisi, uwazi na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wanachama na wadau.   Alisema kuwa mwanachama anaweza kupata huduma mbalimbali zinazotolewa na NSSF bila kulazimika kufika ofisini, ikiwemo, usajili wa wanachama wapya kupitia mfumo ya kidijitali, uwasilishaji na ukusanyaji wa michango ya waajiri na wanachama na kulipa mafao mbalimbali.   Aliongeza kuwa NSSF inashiriki maonesho haya kwa lengo la ...

Mtendaji Mkuu WMA atembelea Maonesho ya Nanenane Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA), Alban Kihulla, leo Agosti 8, 2025 ametembelea Maonesho ya Nanenane kitaifa, katika uwanja wa Nzuguni jijini Dodoma. Akiwa katika Banda la WMA, Afisa Mtendaji Mkuu aliwapongeza watumishi wa Wakala kwa kazi nzuri ya kuelimisha umma ambayo wamekuwa wakiifanya tangu kuanza kwa Maonesho hayo. Aliwataka kuendelea kutoa elimu ya vipimo kwa jamii hata baada ya Maonesho ili wananchi waelewe ni kwa namna gani Serikali kupitia WMA inawalinda kwa kuhakikisha vipimo vinavyotumika katika sekta mbalimbali ni sahihi na vinatumika kwa usahihi. “Tuendelee kutumia majukwaa mbalimbali kutoa elimu ya vipimo kwa wananchi ili waelewe haki yao ya kupata huduma kwa vipimo sahihi lakini pia na wajibu wao wa kuhakikisha wanatumia vipimo sahihi katika sekta mbalimbali” alisema Kihulla. Vilevile, alitembelea mabanda mengine mbalimbali likiwemo banda la Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Taasisi zake ili kujionea huduma zinazot...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maabara Kuu ya Kisasa ya Kilimo iliyopo Mtumba jijini Dodoma

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akitembelea Maabara Kuu ya Kisasa ya Kilimo iliyopo Mtumba jijini Dodoma

Rais, Dkt. Samia azindua Maabara Kuu ya Kisasa ya Kilimo

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Maabara Kuu ya Kisasa ya Kilimo iliyopo Mtumba jijini Dodoma