Posts

Showing posts from November 15, 2025

Mazoezi ni msingi imara kwa Afya bora

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amewataka wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuzingatia afya zao kwa kufanya mazoezi na kufuata kanuni bora za kiafya, ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza ambayo yameendelea kuongezeka katika jamii. Alitoa wito huo mara baada ya kukamilika kwa Mbio za Kuhamasisha Kupima Afya, mbio hizo zilianzia katika O fisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na kuhitimishwa katika Bustani ya Mapumziko ya Nyerere Square, amba p o kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Upimaji Magonjwa y asiyoambukiza kilifanyika. A lisema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha anajilinda dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza. “Nipende kuwasisitiza tu kuwa afya ndio msingi imara na mtaji wa masikini ni nguvu yake mwenyewe . H ivyo , tupambane na tuweke afya zetu vizuri kwa kufanya mazoezi na kupima afya zetu mara kwa mara” alisema Alhaj Shekimweri. Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma , Dkt. Pima Sebastian alisema kuwa...

DC Shekimweri aongoza mazoezi ya Kilomita 5

Image
    Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri apongeza Umoja wa Klabu za Mbio za Pole kwa kujitokeza na kuhamasisha upimaji wa afya na matibabu bure kwa magonjwa yasiyoambukiza.   Mbio hizo zilianzia katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na kuhitimishwa katika bustani ya mapumziko Nyerere Square ambapo maadhimisho hayo ya Wiki ya Upimaji Magonjwa yasiyoambukiza yalitamatika. Alisema kuwa anawashukuru waandaji wa kliniki hiyo kwa kutoa huduma bora. “Siku ya kwanza walipokea wananchi 450 waliojitokeza kupata vipimo na matibabu, jana walihudumia wananchi zaidi ya 300. Kwahiyo, kwa ujumla wamehudumia jumla ya wananchi 1,500. Nimefurahi sana kusikia mwitikio ni mkubwa pia ni imani yetu kuwa baada ya zoezi hili kutamatika, tutafanya upembuzi ili kuona namna tunaweza kufanya zoezi hili kuwa endelevu tukihusishanisha na mazoezi’’ alisema Alhaj Shekimweri. Pia aliwashukuru wananchi wote waliofuatilia Hotuba ya Rais Dkt. Samia waka...