Posts

Showing posts from December 27, 2025

Jiji lataka mpango kazi kukamilisha ujenzi shule ya Mil. 299,200,000 utekelezwe

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imemuagiza Mkuu wa Shule ya Sekondari Nzuguni kusimamia mpango kazi wa ujenzi wa shule mpya ya msingi ya mkondo mmoja yenye gharama ya shilingi 299,200,000 fedha kutoka mradi wa BOOST ili ikamilike kwa wakati kwa mujibu wa mkataba. Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza timu hiyo kutembelea na kukagua hatua ya ujenzi wa shule hiyo katika Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Alisema kuwa mpango kazi wa ujenzi wa shule hiyo unatakiwa kufahamika na kila anayehusika na kusimamia utekelezaji wake ili ujenzi ukamilika kwa wakati. Idadi ya mafundi anatakiwa kuongezeka ili kuhakikisha mradi unakamilika haraka, aliongeza. Pia, ilishauriwa manunuzi yote ya vifaa pamoja na madawati yatangazwe kwenye mfumo wa NeST mapema ili kusiwe na ucheleweshaji katika utekelezaji wa mradi. Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa shule mpya ya msingi mkondo mmoja kwa Ti...

Mwalimu Mkuu S/M Mazengo apongezwa usimamizi ukarabati wa shule

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KASKAZINI Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imempongeza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mazengo kwa kusimamia vizuri ukarabati wa shule kupitia fedha za mradi wa BOOST na kumtaka kuongeza kasi kukamilisha kabla ya shule kufunguliwa ili wanafunzi wasiwe na upungufu wa madarasa ya kusomea. Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza timu hiyo kukagua ukarabati wa shule hiyo jijini Dodoma. Baada ya kupokea taarifa ya ukarabati wa shule hiyo iliyowasilishwa kwa ustadi na mwalimu mkuu na kukagua mradi huo, Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti alisema kuwa mwalimu mkuu (Mwl. Rehema Nkungu) anafanya kazi kubwa na nzuri ya kusimamia ukarabati wa mradi huo. “Hapa kuna ushirikiano mzuri, ninataarifa ya utendaji mzuri wa (Mkaguzi Majengo, Jacob Stephen) anayesimamia mradi huu tangu nikiwa ofisini, hongera sana. Matamanio yetu, kasi iongezeke ya ukarabati huu ukamili...

Menejimenti ya Jiji la Dodoma yaelekeza ukarabati S/M Dodoma Mlimani kufanyika usiku na mchana

Image
Na. Dennis Gondwe, TAMBUKARELI Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani ametakiwa kusimamia ukarabati wa madarasa 12 kufanyika hadi usiku ili ukamilike mapema kabla ya shule kufunguliwa kwa sababu fedha shilingi 150,000,000 zimeshatolewa. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ukarabati wa madarasa 12 kwa shilingi 150,000,000 fedha kutoka mradi wa BOOST. Alisema kuwa kazi ya ukarabati inatakiwa kufanyika usiku na mchana ili kukamilisha madarasa hayo kwa wakati. Aliongeza kuwa fedha ipo, hivyo, hakuna sababu ya kufanya mradi uchelewe kukamilika, na kuwataka afisa mtendaji kata na mtaa kuweka kambi shuleni hapo kusimamia utekelezaji wa ukarabati wa shule hiyo.    Akiongelea mradi huo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Dodoma Mlimani, Mwl. Jenipher Mhavile alisema kuwa ukarabati ulianza 13 Oktoba, 2025. “Hatua ya ukara...

Chidachi S/M watakiwa kuboresha mpango kazi wa fundi kukamilisha ujenzi mradi wa BOOST

Image
Na. Dennis Gondwe, MKONZE Mhandisi wa halmashauri, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chidachi wametakiwa kufanya mapitio ya mpango kazi wa mafundi na kuandaa mpango wa haraka unaotekelezeka ili kukamilisha mradi wa ujenzi wa miundombinu kwa gharama ya shilingi 182,100,000 fedha kutoka mradi wa BOOST shuleni hapo. Agizo hilo lilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoambatana na Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kukagua ujenzi wa mradi wa miundombinu katika Shule ya Msingi Chidachi kwa fedha za ufadhili wa BOOST. Timu ya Menejimenti ilipokagua mradi huo haikuridhika na kasi ya ujenzi na kuelekeza mhandisi wa halmashauri, mwalimu mkuu pamoja na fundi kupitia upya mpango kazi na kutengeneza mpango kazi wa haraka unaotekeleza ili kukamilisha mradi huo kwa wakati uliopangwa. Mkurugenzi alisema kuwa kila mmoja anatakiwa kuongeza umakini katika usimamizi ili mradi ukamilishwe kwa viwango, na kusema kuwa menejimenti haitachele...

Jiji la Dodoma lataka kasi ukarabati madarasa Kitelela Sec

Image
Na. Dennis Gondwe, NZUGUNI TIMU ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeelekeza kuongeza kasi ya ukamilishaji wa ukarabati wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kitelela ili wanafunzi watakapofungua shule mwezi Januari, 2026 waweze kuyatumia. Agizo hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza timu hiyo kutembelea na kukagua maendeleo ya ukamilishaji wa ukarabati wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kitelela iliyopo Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Dkt. Sagamiko ambae ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa baada ya kukagua hali ya ukarabati inavyoendelea, kasi siyo ya kuridhisha. “Hivyo, maelekezo yetu ni kwamba, kasi iongezeke ili mradi ukamilike kwa wakati na shule zinapofunguliwa wanafunzi waanze kutumia madarasa hayo” alisema Dkt. Sagamiko. Wakati huohuo, alimuagiza Afisa Mtendaji wa Kata ya Nzuguni na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Kitelela kuweka kambi katik...

Diwani Iyumbu apongezwa usimamizi miradi

Image
Na. Dennis Gondwe, IYUMBU DIWANI wa Kata ya Iyumbu amepongezwa kwa kusimamia miradi ya maendeleo na kutakiwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa wataalam wa kata hiyo ili kukamilisha miradi kwa wakati ili iweze kutoa huduma kwa wananchi. Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipoongoza Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji kutembelea na kukagua ukamilishaji wa madarasa mawili, maabara tatu, jengo la utawala na matundu nane ya vyoo katika Shule ya Sekondari Iyumbu. “Mheshimiwa Diwani ninakupongeza kwa kusimamia vizuri miradi katika Kata ya Iyumbu. Kwa umoja huu kata inakwenda kubadilika kimaendeleo, wape ushirikiano wataalam katika kata ili kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kwa nafasi yako upo katika wakati mzuri zaidi kuhamasisha wananchi kujitolea kushiriki shughuli za maendeleo na nguvu kazi” alisema Dkt. Sagamiko. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Iyumbu, Sadick Mpondamali aliishukuru halmashauri kwa kut...