Jiji la Dodoma kinara utekelezaji afua za Lishe
Na. Mwandishi wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepata alama ya kijani katika kadi alama ya viashiria vya utekelezaji wa afua za lishe ikiwa ni hatua nzuri kwa kipindi cha Robo ya Nne kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026. Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Lishe kwa kipindi hicho, Kaimu Afisa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Happiness Mlamka alisema kuwa utekelezaji umeendelea kufanyika kwa mafanikio makubwa ambapo kadi alama ya lishe imeonesha rangi ya kijani. Alisema kuwa rangi hiyo ni kiashiria kwamba halmashauri imefikia viwango vinavyotakiwa katika utekelezaji wa afua za lishe. Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wake, Sakina Mbugi, aliyemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Dodoma alipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuendelea kufanya vizuri katika utekelezaji wa shughuli za lishe. Alisisitiza umuhimu wa kuendeleza utoaji wa elimu ya lishe kwa kutumia kaulimbiu mbalimbali zinazotolewa kupitia Mbio za Mwenge wa Uhuru, ikiwemo “Zingatia lishe yak...