Posts

Showing posts from February 26, 2025

DC Shekimweri awaasa viongozi kutokuchukulia mzaha suala la madada poa

Image
Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, alitoa maoni kwa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kufanya utafiti, kutoa elimu na kuweza kujua sababu zinazowafanya wanawake na vijana kufanya biashara ya ngono. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri Aliyasema hayo wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa kazi robo ya pili kwa kipindi cha Mwezi Oktoba hadi Desemba, 2025 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alhaji Jabir Shekimweri alisema ā€œHalmashauri ya Jiji la Dodoma ina mifuko mahsusi ya vijana na wanawake, hivyo uchunguzi ufanyike kujua kwanini matendo ya uzinifu yanaendelea. Katika kutafuta suluhisho pengine Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, ingawa taarifa ilipitishwa sioni kama vita ya biashara hiyo ya watu kujiuza katika shughuli za ngono haihitaji ā€˜cohesive forceā€™ nguvu ya dola, nadhani inahitaji elimu zaidi na mikakati ya k...

Shekimweri awaita mashabiki wa Dodoma Jiji FC, Ally Hassan Mwinyi

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameitakia kila la kheri timu ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wao ujao dhidi ya Tabora United FC, utakaopigwa katika dimba la Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri akielezea jambo Alizungumza hayo wakati akitoa salamu katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. ā€œLicha ya changamoto timu yetu iliyopitia, timu imeweza kufanya vizuri katika michezo miwili mtawalia. Timu hii ni fahari ya nchi ikiiwakilisha makao makuu ya nchi. Hivyo, tunawatakia kila la kheri katika mchezo wao dhidi ya Tabora United FC watakaocheza ijumaa. Tunawasisitiza wadau na wana Dodoma kwenda kuipa nguvu timu yetu ili matokeo yawe mazuriā€ alisema Shekimweri. Naye, Elice Kitendya alisema ā€œkwakua mimi ni mdau mkubwa wa timu yetu ya Dodoma Jiji, nina matumaini makubwa na timu yetu, mashabiki tunawahimiza wenye nafasi ya kwenda Tabora tujumuike pamoja kwenda kuisa...

DC Shekimweri awaasa viongozi kutokuchukulia mzaha suala la madada poa

Na. Shahanazi Subeti, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, alitoa maoni kwa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kufanya utafiti, kutoa elimu na kuweza kujua sababu zinazowafanya wanawake na vijana kufanya biashara ya ngono. Aliyasema hayo wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa kazi robo ya pili kwa kipindi cha Mwezi Oktoba hadi Desemba, 2025 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alhaji Jabir Shekimweri alisema ā€œHalmashauri ya Jiji la Dodoma ina mifuko mahsusi ya vijana na wanawake, hivyo uchunguzi ufanyike kujua kwanini matendo ya uzinifu yanaendelea. Katika kutafuta suluhisho pengine Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, ingawa taarifa ilipitishwa sioni kama vita ya biashara hiyo ya watu kujiuza katika shughuli za ngono haihitaji ā€˜cohesive forceā€™ nguvu ya dola, nadhani inahitaji elimu zaidi na mikakati ya kuwafikia hao na pengine kuwabadilishaā€. Pia, a...

Wananchi Dodoma watakiwa kuzingatia vibali vya ujenzi

Na. Halima Majidi, VIWANDANI Wananchi jijini Dodoma wametakiwa kuacha tabia ya ujenzi wa aina yoyote bila ya kufuatilia vibali kwa sababu ni kosa la kisheria na linaweza kusababisha ujenzi holela na migogoro ya Ardhi isiyo ya lazima. Hayo yalisemwa na Msanifu Majengo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Paschal Mathew wakati akitoa elimu juu ya umuhimu wa vibali vya ujenzi kwa wananchi wanaotaka kujenga ikiwa ni muendelezo wa Kliniki ya Ardhi inayofanyika jijini hapo katika viwanja vya iliyokuwa Manispaa ya zamani. Alisema kuwa vibali vya ujenzi wanatoa kwa mujibu wa sheria, na kwa viwanja vyote ambavyo vimeshafanyiwa vipimo na kumilikishwa ili mwananchi apewe huduma, lazima awe na nyaraka za umiliki pamoja na michoro ya majengo anayotaka kuendeleza yakizingatia matumizi na sheria ndogo za Halmashauri ya Jiji la Dodoma. ā€œTunakagua michoro kuangalia kama imekamilika na imekidhi vigezo vya kihandisi na kisanifu na kuwaandikia ā€œinvoiceā€ kwaajili ya kufanya malipo ya kibali cha ujenzi. ...