Posts

Showing posts from July 3, 2026

Afisa Biashara Arusha apongeza ukuwaji wa Biashara wa Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM   HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa kasi ya ukuaji wa shughuli za biashara na uwekezaji na kutajwa kuwa ni fursa kwa watanzania na wageni kuwekeza.   Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji Halmashauri ya Jiji la Arusha, John Kilunge alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Kilunge alipongeza kasi ya ukuaji wa shughuli za biashara na uwekezaji ndani ya jiji hilo na kusema kuwa ni fursa kwa watanzania na wageni kuwekeza na kufungua zaidi fursa za ajira. Akiwa katika banda hilo, alipata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo, hususan katika sekta za ardhi, biashara na maendeleo ya kiuchumi. Alisema kuwa Jiji la Dodoma linaonesha mafanikio makubwa katika kukuza mazingira ya biashara na kuvutia wawekezaji k...

Jiji la Dodoma lashauriwa kulinda hadhi ya Makao Makuu ya Nchi

Image
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM   HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeshauriwa kuendelea kusimamia Mpango Kabambe wake ili kuhakikisha jiji linakuwa na mpangilio wa kisasa na kulinda hadhi ya makao makuu ya nchi.   Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo (kushoto) akiongea na wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Julius Nyerere jijini hapa.   Alisema kuwa ukuaji wa Jiji la Dodoma unapaswa kwenda sambamba na upangaji bora wa maeneo, miundombinu na mazingira ya mji ili kuongeza mvuto zaidi kwa wakazi, wawekezaji na wageni wanaofika kwa shughuli mbalimbali za kiserikali na kiuchumi.   Alisisitiza kuwa taswira ya mji ambao ni makao makuu ya nchi inapaswa kuonekana wazi kupitia mpangilio wa kisasa, unaozing...