Posts

Showing posts from November 23, 2023

KAMATI YA SIASA KATA YA MSALATO YATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI

Image
  Na. Dennis Gondwe, MSALATO KAMATI ya Siasa ya Kata ya Msalato imetakiwa kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika kata ili kujiridhisha ya thamani ya fedha. Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Charles Mamba alipoongoza Kamati ya Siasa Wilaya ya Dodoma kutembelea na kukagua ujenzi wa mabweni mawili, vyumba saba vya madarasa na matundu 10 ya vyoo katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Msalato iliyopo Kata ya Msalato jijini hapa. Mamba alisema kuwa Kamati ya Siasa Kata ya Msalato ina wajibu wa kufuatilia na kusimamia miradi yote ya maendeleo inayotekelzwa katika kata hiyo. “Kamati ya Siasa Kata ya Msalato mradi huu ni wa kwenu, msisubiri Kamati ya Siasa Wilaya ya Dodoma kuja kukagua. Lazima muwe mnapanga ratiba zenu kukagua miradi hii. Serikali ya awamu ya sita inaleta fedha nyingi kwenye kata kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo, jukumu lenu ni kusimamia utekelezaji wake na thamani ya fedha ionekan...

KAMATI YA SIASA WILAYA YA DODOMA YAPONGEZA UJENZI KITUO CHA AFYA ILAZO

Image
  NA. Dennis Gondwe, ILAZO KAMATI ya Siasa ya Wilaya ya Dodoma imeridhishwa na hatua ya ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo unaoendelea na kusema kuwa wilaya inaoga maendeleo. Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Dodoma wakikagua ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma, Charles Mamba alipoongoza Kamati ya Siasa Wilaya ya Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo kinachojengwa jijini Dodoma. Mamba alisema “nianze kwa kumshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuitendea mema Dodoma hasa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Sisi tunaoga maendeleo. Kata ya Nzuguni, Ipagala na kata za jirani. Mradi huu ni wenu na ni jukumu lenu kuutunza ili uwe endelevu”. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma, Shaban Shaban alisema kuwa wasimamiz wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ilazo wapo makini. “Kwa jinsi tulivyoukagua tu mradi tumeona kuta zimenyooka vizu...