Jiji la Dodoma kutekeleza mradi wa urejeshaji taka
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya JUZA, Nasibu Kitabu kwa kushirikiana na Kampuni ya Global Waste Solutions watambulisha mradi wa uchakataji na urejeshaji wa taka kwa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kupunguza kiwango cha taka zinazopelekwa katika Dampo la Chidaya. Aliyazungumza hayo katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri na kusema kuwa taasisi hiyo imejikita katika uhifadhi na utunzaji wa mazingira pamoja na kutoa elimu kwa vijana wanaofanya kazi ya kuzoa taka. “Kwasasa tupo katika Jiji la Dodoma na tumeungana na Global Waste Solutions kufanya hii kazi ili kupunguza kiasi kikubwa cha taka kwenda dampo ifikapo mwaka 2027. Yote hii ni kuweza kuifundisha jamii namna ya kutenganisha taka ili tuweze kuiokoa jamii yetu na changamoto zitokanazo na utunzaji na utupaji holela wa taka” alisema Kitabu. Aliongeza kuwa Jiji la Dodoma limekuwa kwa kasi na ndipo ilipo sura ya nchi. “Jili la Dodoma ni fahari ya watanzania, tumeona ni vem...