Posts

Showing posts from July 8, 2023

TANZANIA NA KOREA KUSINI KUSHIRIKIANA UTAFITI WA KILIMO NA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KILIMO

Image
Nchi za Tanzania na Korea Kusini zimekubaliana kushirikiana katika kuimarisha utafiti wa kilimo na matumizi ya teknolojia ya kisasa ya kilimo ili kuongeza tija kwa wakulima wa Tanzania. Hayo yamesemwa leo Mjini Jeonju-si, Korea Kusini wakati wa mazungumzo ya ushirikiano baina ya Naibu Waziri wa Kilimo wa Tanzania, Mh. Anthony Mavunde na Ndg. Yun Jongchul Makamu Mtawala Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Kilimo na Utafiti ya Korea (Korea Patnership for Innovation in Agriculture- KOPIA). Kupitia mazungumzo hayo Naibu Waziri Mavunde ameiomba KOPIA kuanzisha kituo chake nchini Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI) ili kubadilishana uzoefu na kuongeza ufanisi katika tafiti za kilimo kwa lengo la kumsaidia mkulima kulima kwa tija na kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kwa kutumia kanuni bora za kilimo,uzalishaji mbegu bora na teknolojia ya kisasa ya kilimo,sambamba na hayo Naibu Waziri Mavunde ameomba pia ushirikiano wa kitaalamu katika utekelezaji wa P...

WANANCHI KATA YA CHAMWINO WASHIRIKI USAFI WA PAMOJA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WANANCHI wa Kata ya Chamwino wajitokeza kushiriki usafi wa Mazingira wa kila Jumamosi kwa lengo la kuweka Mazingira safi yanayowazunguka na kujiepusha magonjwa yanayosababishwa na uchafu wa Mazingira. Akiongelea lengo la wananchi wa kata hiyo kufanya usafi wa pamoja wa Mazingira, Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa ni kuhakikisha Mazingira ya kata hiyo yanakuwa safi. “Kata ya Chamwino, usafi ni tabia yetu. Muitikio wa wananchi kujitokeza kushiriki katika usafi wa pamoja ni mkubwa unaolenga kuweka Mazingira safi. Muitikio huo pia ni utekelezaji wa maagizo ya viongozi wetu kuelekeza tufanye usafi wa Mazingira ili kujihakikishia Mazingira safi na kuepuka magonjwa yanayotokana na uchafu wa Mazingira” alisema Nkelege. Alisema kuwa usafi ulifanyika katika maeneo mbalimbali ukijumuisha usafi wa mitaro ya maji ya mvua, maeneo ya biashara na maeneo ya makazi. “Maeneo haya ni muhimu kwa sababu yanatumiwa na wananchi wengi kupata huduma” ...