Posts

Showing posts from January 30, 2025

Sekta binafsi kugharamia miradi Jiji la Dodoma Bajeti ya 2025/2026

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Sekta binafsi itashiriki kugharamia miradi ya maendeleo kwa njia ya ubia katika utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kutokana na umuhimu wa sekta hiyo kwa maendeleo ya Jiji la Dodoma. Katibu wa Baraza la Madiwani, Dkt. Frederick Sagamiko Mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, imeshirikisha sekta binafsi kutokana na matamanio na mahitaji kuwa makubwa kuliko makusanyo ya mapato. Hayo yalisemwa na Katibu wa Baraza la Madiwani ambaye ni Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, alipokuwa anatolea ufafanuzi katika baadhi ya masuala yaliyowasilishwa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani maalum kwa ajili ya kupokea na kupitia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma tarehe 30 Januari, 2025. Dkt. Sagamiko alisema “ matamanio yetu na mahitaji yetu ni makubwa kul...

Wananchi Dodoma wahimizwa kutunza Mazingira

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkuu wa Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro, alisema kitengo kicho kimejipanga kikamilifu katika kuendelea kutekeleza shughuli mbalimbali za udhibiti na uondoshaji wa taka ili kuhakikisha Jiji la Dodoma linakuwa katika hali ya usafi na kuvutia. Aliyasema hayo nje ya Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la kupitia rasimu ya Mpango na Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumzia kuhusu udhibiti wa taka ngumu, Dickson Kimaro, alisema kupitia bajeti iliyotengwa na halmashauri, kitengo hicho kinajiandaa na mchakato wa kununua mitambo maalum kwaajili ya kuchakata takataka na kuwepo kwa gari ili kukusanya na kupeleka eneo la dampo kuu la Chidaya. “Tunatarajia kwenda kununua mitambo ya kuchakata takataka, lakini kununua malori kwaajili ya uondoshaji wa taka ili kuondokana na mfumo wa ‘Collection Point’, bali kuchuku...

Sekta ya Michezo yaguswa Bajeti 2025/2026 Halmashauri ya Jiji la Dodoma

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepanga kujenga viwanja vya michezo ikiwemo uwanja wa mpira wa miguu uliopo katika mchakato wa ujenzi, kuelekea michuano ya Mataifa ya Afrika (Afcon) 2027 ambapo kwa pamoja nchi za Afrika Mashariki Tanzania, Kenya na Uganda zitakuwa wenyeji wa michuano hiyo. Mpango huo umewekwa wazi na Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Francis Kaunda kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt.   Frederick Sagamiko, wakati akiwasilisha Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Baraza Maalum la Madiwani, lililofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kwa upande wake Daudi Fundikira, Diwani wa Kata ya Chang'ombe baada ya kupitishwa kwa Bajeti hiyo alisema "Tumepanga kujenga viwanja vya michezo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambavyo vitakua ni sehemu ya kuongeza mapato kwa jiji letu la Dodoma, lakini pia ni fursa kwa vijana wetu kufanya mazoezi na kuweza kuonekana, kwani michezo ni ajira na mic...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma launga mkono maono ya Rais Dkt. Samia Nishati safi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inaunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha nishati safi kwa wote inapatikana kwa lengo la kuboresha maisha ya watanzania. Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Prof. Davis Mwamfupe alipokuwa akifungua mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili na kupitia mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/ 2026 mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Prof. Mwamfupe alisema “ sisi Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma tunatoa pongezi kwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa nishati safi. Mwanzo mwa wiki hii dunia yote macho yalikuwa Tanzania kwa ajili ya mkutano wa nishati kwa ajili ya afya kwa manufaa ya wananchi wetu na mazingira bora. Dodoma ni wanufaika wakubwa wa dhana hiyo kwasababu miti yetu itabaki salama. Sisi ni waungaji mkono namba moja wa dhana hii ”. ...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapitisha Bajeti 2025/2026 shilingi bil. 147

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma lapitisha kwa kauli moja rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 jumla ya shilingi bilioni 147.9 ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.04 ukilinganisha na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2024/2025. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri wa jiji hilo, ambao ulilenga kupitisha mapendekezo ya rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026. Akiwasilisha rasimu hiyo, Mchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Francis Kaunda, alisema kuwa h almashauri imekasimia kukusanya shilingi bilioni 67.3 kati ya fedha hizo bilioni 43 ni mapato yasiyolindwa na shilingi 24.3 ni mapato lindwa, ambapo halmashauri ipo kwenye kundi ambalo asilimia 70 ya mapato yasiyolindwa inayoelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 30 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Alisema kuwa, rasimu ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2025/2026 itagharamiwa na vyanzo vikuu vinn...