Posts

Showing posts from September 20, 2024

Mbunge Mavunde awakumbuka mama lishe Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini Anthony Mavunde, ameahidi kuwatengenezea mazingira mazuri na rafiki ya kufanyia biashara mama lishe waliopo pembezoni mwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. Mavunde alizungumza hayo mara baada ya kumaliza zoezi la uzinduzi wa ujenzi wa jengo la kupumzikia wananchi lilipo nje ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma. Aidha, Mavunde aliahidi kuwaboreshea na kuwatengenezea mazingira rafiki ya kufanya biashara ya chakula na kukarabati miundombinu kama vile kuwatengenezea meza na viti za kufanyia biashara pamoja na kuweka maeneo nadhifu. Mavunde alisema “sambamba na hilo nafahamu ya kwamba, asilimia kubwa ya wanaokaa pale hawavimudu vyakula ambavyo watu wengi hapa tunavimudu vyakula vya mahotelini...”. Hata hivyo, Mavunde aligusia wananchi wa kipato cha chini wasioweza kumudu gharama kubwa za kununua chakula kwa ajili ya wagonjwa wao hivyo kuahidi kuwasaidia mama lishe kuboresha maeneo yao ya kufanyia kazi kuwa safi na sal...

Mkuu wa Wilaya Apongeza Ujenzi wa Madarasa Mtumba

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, ametembelea miradi ya serikali iliyopo Kata ya Mtumba na kusisitiza elimu kuwa agenda ya kudumu. Akizungumza na walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mtumba alitoa wito kwa jamii kufuatilia kwa karibu maendeleo ya kitaaluma, ufundishaji na ujifunzaji ili kuhakikisha majengo mazuri yaliyojengwa yanaakisi ubora wa elimu. Alisema kuwa ni muhimu katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata elimu bora na yenye tija, na kwamba walimu wana nafasi kubwa katika kufanikisha hilo. “Nisisitize agenda hii ya elimu iwe ni ya kudumu, fuatilieni kwa karibu maendeleo ya kitaaluma, ufundishaji ili kusudi majengo haya mazuri tuliyojengewa yaakisi katika ubora wa elimu” alisema Alhaj Shekimweri. Aidha, aliwapongeza walimu kwa kazi nzuri wanayoifanya na kuwataka waendelee kuwafundisha watoto kwa upendo na kwa kuwajali ili kuwasaidia watoto kujifunza vizuri bila kuhofia chochote. “Walimu muwafundishe watoto kwa upendo, muwaele...

Mtumba yapata madarasa mapya kwa kidato cha Tano na Sita

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha kuwa watoto wanapata elimu bora na kufuatiliwa kwa karibu ili wafaulu. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akitoa wito kwa Jumuiya ya Shule ya Sekondari Mtumba Aliyazungumza hayo katika ziara ya kutembelea mradi wa ujenzi wa madarasa nane na matundu 10 ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Mtumba jijini Dodoma. Alhaj Shekimweri alisisitiza umuhimu wa kuwapeleka watoto shule na kusimamia maendeleo yao ili kuwawezesha kufaulu kwa kiwango cha juu. “Tupeleke watoto wetu shule na sio tu kuwapeleka shule, tuwasimamie pia wafaulu. Kama dhamira ni kufanya watoto wetu wasome hapahapa, ni vema waje na watoto wa nje wajichanganye na watoto wetu ili kufundishana tamaduni mbalimbali na tutajenga watanzania wenye umoja” alisema Alhaj Shekimweri. Mkuu wa Wilaya alisisitiza pia umuhimu wa kuweka uzio kwenye shule hiyo ...