Posts

Showing posts from August 6, 2025

TAKUKURU yapewa rai kuboresha mikakati ya kutokomeza rushwa

Image
Na. Nancy Kivuyo , DODOMA Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imeeleza kuwa katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania imejipanga kutoa elimu na kusisitiza wananchi kuepuka kupokea rushwa kwaajili ya kuchagua viongozi. Hayo yalielezwa na Mratibu wa Banda la TAKUKURU, Suzana Raymond wakati akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma aliyetembelea banda hilo katika maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea Nzuguni jijini Dodoma. Alisema kuwa banda la TAKUKURU limejikita katika kutoa elimu na kupokea taarifa zinazohusu masuala ya rushwa. “ Pamoja na majukumu yote, wakati mwingine tunapokea ushauri mbalimbali kwasababu sisi tunaweza tusione tunachokifanya lakini walio nje ndio wanaona nini tunakifanya na huwa tunapeleka ngazi za juu na wao wanazifanyia kazi kwa kadri inavyotakikana ” alisema Raymond . Alisema k u wa lengo la kuwepo katika maonesho ya Nanenane ni kuhakikisha wanatoa elimu ya kutosha kwa jamii hasa kuelekea uchaguzi mkuu. “Lakini katika...

DC Shekimweri ashauri TMDA kuwa wabunifu

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj. Jabir Shekimweri, ameitaka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kuwa wabunifu na kutumia teknolojia ya kisasa katika shughuli zake za ukaguzi wa dawa na vifaa tiba nchini, ili kuongeza ufanisi na kuimarisha usalama wa wananchi. Alisema hayo wakati alipotembelea banda la TMDA katika Maonesho ya Wakulima Nane n ane yanayofanyika katika viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma. Alisema kuwa an a wapongeza kwa kuendelea kutoa huduma ikiwemo kusajili, kudhibiti na kufuatilia ubora wa dawa . “Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kulinda afya za wananchi kupitia udhibiti wa dawa na vifaa tiba. Hata hivyo, katika dunia ya sasa ya teknolojia, mnapaswa kuwa wabunifu zaidi katika mbinu zenu za ukaguzi ili kuweza kufika maeneo mengi kwa haraka na kwa ufanisi zaidi na kuendele a kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi sahihi ya dawa” alisema Alhaj. Shekimweri. P ia aliongezea kwa kuwasisitiz a kuendelea kushirikiana kwa karibu na vyombo ...

Teknolojia Bunifu ya Mifugo yasogezwa maonesho ya Nanenane

Image
Na. Husna Rajabu, DODOMA Taasisi ya Wakala wa vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) imeteka umakini wa wageni katika maonesho ya Nanenane jijini Dodoma kwa kuonesha teknolojia bunifu zinazolenga kuongeza thamani ya mazao ya mifugo na kuboresha maisha ya wafugaji. Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Idara ya Utafiti na Huduma za Ushauri (LITA), Joseph Msemwa, alisema kuwa taasisi hiyo imeweka bayana bidhaa na huduma kadhaa ambazo ni matokeo ya kazi za vijana wa kitanzania. Alisema kuwa maonesho ya Nanenane ni sehemu muhimu ya kuonesha bidhaa na teknolojia zitakazobadilisha taswira ya uchumi wa wananchi. “Tupo hapa kwenye maonesho ya Nanenane jijini Dodoma, tumeleta teknolojia mbalimbali zinazohusiana na bidhaa za maziwa. Pia tuna teknolojia ya uchakataji wa ngozi ambapo tunawafundisha vijana wetu namna ya kuchakata ngozi, kuanzia ikiwa mbichi mpaka ifike hatua ya mwisho ya utengenezaji wa bidhaa. Kama mnavyojionea bidhaa za ngozi zipo za aina tofauti tofauti ikiwemo viatu, heren...

Sura mpya ya kilimo cha vitunguu yaonesha mafanikio

Image
Na. Husna Rajabu, DODOMA Kitunguu kimekuwa ni miongoni mwa zao la biashara chenye faida kubwa na hulimwa karibu maeneo yote nchini hasa maeneo ya miinuko ya kaskazini mwa Tanzania. Katika maonesho ya wakulima Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma vipando bustani vya Halmashauri ya Jiji la Dodoma vimejumuisha teknolojia ya ulimaji vitunguu kwa njia ya asili katika eneo dogo na kupata mazao mengi. Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Madei Kidai alieleza mchakato wa kilimo hicho chenye tija kibiashara. “Ili kufanikisha kilimo cha vitunguu, ni lazima uanze na maandalizi ya shamba. Pia, tunawahimiza wakulima kutafuta mbegu bora, kuandaa matuta vizuri, na kuhamisha miche kutoka kwenye kitalu baada ya muda muafaka. Hapa kwetu tumetumia mbinu hizi, na matokeo yanaonekana kama hivi mnavyoona” alieleza Kidai. Kwa mujibu wa Kidai, baada ya kupanda, hatua muhimu zinazofuata ni umwagiliaji na udhibiti wa wadudu na magonjwa. Alisisitiza kuwa wametumia v...

Dodoma Jiji FC yatangaza benchi la ufundi msimu wa 2025/2026

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imemtambulisha Mashami Vicent raia wa Burundi kuwa kocha wake mkuu kuelekea kwenye msimu wa mashindano ya ligi kuu ya NBC msimu wa mwaka 2025/2026, sanjari na hilo imemtambulisha Bakira Guy raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwa kocha msaidizi wa klabu hiyo. Hayo yalibainishwa na Novatus John, Mtendaji Mkuu wa Dodoma Jiji FC, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Vizano jijini Dodoma ukiwa na lengo la kutambulisha benchi jipya la ufundi. “Baada ya kuvunja benchi letu zima la ufundi tulilokuwa nalo msimu uliopita, kama uongozi tulikaa chini na kuanza mchakato rasmi wa kutafuta benchi jipya la ufundi. Tulikuwa makini kupitia “CV” za makocha mbalimbali hatimae tukaweza kupata kocha bora zaidi ya wote na ndiye huyu ambaye tumemtangaza. Kwa upande wetu tutampatia stahiki zake zote ili timu yetu ifanye vizuri zaidi msimu ujao” alisema John. Mashami Vicent kabla ya kutuwa Dodoma J...