Vijana Dodoma na Iringa Kukutana Kupaza Sauti Dhidi ya Rushwa
Na. Muhamad Said, IRINGA Wanafunzi kutoka klabu za wapinga rushwa za shule za msingi na sekondari za mikoa ya Dodoma na Iringa leo wanatarajiwa kukutana katika mdahalo maalumu wa mapambano dhidi ya rushwa. Mdahalo huo utafanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Lugalo, mkoani Iringa, ukilenga kuwajengea wanafunzi uelewa, kuimarisha maadili na kuongeza ushiriki wa vijana katika mapambano dhidi ya rushwa ndani ya shule na jamii kwa ujumla. Kupitia mdahalo huo, wanafunzi wanatarajiwa kutoa hoja kuhusu madhara ya rushwa kwa jamii na taifa pamoja na changamoto zinazoweza kujitokeza katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo. Aidha, mjadala unatarajiwa kutoa nafasi kwa vijana kueleza namna wanavyoweza kuwa sehemu ya mabadiliko katika kujenga jamii inayozingatia uadilifu. Ushirikishwaji wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari unatarajiwa pia kuifanya shughuli hiyo kuwa sehemu ya kuwaandaa vijana kuwa mabalozi wa maadili na mapambano dhidi ya rushwa, kwa kuanza kujenga uelewa na msi...