Posts

Showing posts from October 2, 2024

Twende Butiama kupambana na ujinga, umasikini na maradhi Jiji la Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA MAKULU Waendesha baiskeli wamuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Nyerere kwa lengo la kupambana na maadui watatu wa maendeleo ambao ni maradhi, umasikini na ujinga kwa kugawa madawati 100 katika Shule ya Msingi Dodoma Makulu iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Mwenyekiti wa msafara Twende Butiama Gabriel Landa, alisema kuwa msafara huo una lengo la kumuenzi Baba wa Taifa kwa vitendo kwasababu Mwl. Julius Nyerere alitumia chombo cha baiskeli wakati alipokuwa mwalimu na hata alipoacha uwalimu na kuanza harakati za kupigania uhuru na mambo mbalimbali alitumia baiskeli. Mwalimu Nyerere pia aliwahi kusafiri kwa kuendesha baiskeli kutoka Dar-es-Salaam hadi Arusha, aliongeza. Msafara huo umewaunganisha watu wa nchi mbalimbali kwa kuonesha Mwalimu Nyerere alikuwa sio mbinafsi bali mpenda umoja. “Wengi wanaotuona barabarani wanahisi haya ni mashindano ila haya sio mashindano bali ni msafara wa kawaida ambao tunaendesha baiskeli kwa mwendo wa upendo am...

Twende Butiama wakabidhi Madawati 100 SM Dodoma Makulu

Image
Na. Asteria Frank, DODOMA MAKULU   Watu wasiopungua 90 washiriki kwenye msafara wa Twende Butiama wakiendesha baiskeli kutoka Dar-es-Salaam na kwenda Butiama kwa lengo la kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Nyerere waliwasili jijini Dodoma katika Shule ya Msingi Dodoma Makulu na kugawa madawati 100 na kushiriki zoezi la kupanda miti.   Msafara huo ulianza safari tarehe 30 Septemba kutoka Dar-es-Salam na unatarajiwa kufika Butiama tarehe 13 Oktoba, 2024 ukidhaminiwa na Vodacom pamoja na Benki ya Stanbic walikabidhi madawati 100 na kupanda miti katika Shule ya Msingi Dodoma Makulu.   Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Kaspar Mmuya aliupokea msafara huo wa Twende Butiama na alisema kuwa, upandaji miti unaunga falsafa ya kutunza Mazingira. Alisema kuwa utoaji wa madawati shuleni unaugana na falsafa ya Mwl. Julius Nyerere ya kuangamiza maadui watatu wa maendeleo ikiwemo ujinga, umasikini na maradhi.   Alisema kuwa, kitendo wanachofanya ni kizuri kwa Tanz...

Naibu Meya Chibago afurahia Kampeni ya Upandaji Miti Dodoma

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA MAKULU Naibu Meya wa Halmashauri Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago amefarijika na kampeni ya upandaji miti inayofanywa na wanariadha wanaotumia baiskeli katika kuzienzi falsafa za Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere ya kupambana na adui wa maendeleo kwa kuondoa ujinga, maradhi na umasikini. Naibu Meya wa Halmashauri Jiji la Dodoma, Fadhili Chibago akielezea kufurahia kampeni ya upandaji miji  Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akimkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa, Kaspar Mmuya katika zoezi la upandaji miti na ugawaji madawati katika Shule ya Msingi Dodoma Makulu, jijini Dodoma lililofanywa na wanariadha kutokea Dar es Salaam wakielekea Butiama. Chibago alisema kuwa amefarijika sana na kampeni ya wanariadha hao wa kuendesha baiskeli, upandaji miti ikiwa ni falsafa moja wapo ya kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Nyerere katika falsafa zake tatu za kupambana na maadui wa maendeleo ambao ni ujinga, umaskini na maradhi. “Jiji la Dodoma tumefarijika sana na ka...