Posts

Showing posts from August 3, 2025

Afisa Biashara Jiji la Dodoma aelezea umuhimu wa kuanzisha Kanda za Huduma

Image
Na. Ramla Makamba, HOMBOLO BWAWANI Katika kuhakikisha huduma za mapato zinapatikana kwa urahisi na kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato halmashauri ya Jiji la Dodoma imeanzisha mfumo wa kanda zitakazohudumia wakazi wa kata mbalimbali kwa karibu ambapo wataalamu watakuwa katika maeneo mbalimbali kutoa huduma hizo zikiwemo huduma za ukataji wa leseni ambapo mpango huo utaanza mapema mwezi Agosti, 2025. Wananchi watapata huduma kama vile za ulipaji wa tozo mbalimbali katika maeneo yao bila kulazimika kufuata huduma Katikati ya jiji ikiwa ni miongoni mwa harakati za kutatua changamoto za umbali wa upatikanaji wa huduma pamoja na kuhakikisha ukusanyaji thabiti wa mapato ya serikali ambapo mwanzoni yalikuwa hayafanywi kikamilifu. Hayo yalisemwa na Afisa Biashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Fikiri Mtoi, katika kikao kilichofanyika Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo Bwawani jengo la utawala, na kuhudhuriwa na watendaji wa kata, watendaji wa mitaa, wenyeviti wa mitaa na wadau wa b...

Wenyeviti Serikali za Mitaa Hombolo Bwawani wapewa mafunzo huduma ndogo za kifedha

Image
Na. Rehema Kiyumbi, HOMBOLO BWAWANI Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Halmashauri ya Jiji la Dodoma latoa elimu kwa wananchi wa Kata ya Hombolo Bwawani juu ya matumizi ya fedha na kuweka akiba kwa lengo la kujikwamua kiuchumi. Akizungumza na wananchi wa kata hiyo, Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Hidaya Abdallah alisema kuwa elimu ya huduma za kifedha ni muhimu kwa wananchi ili kuweza kufahamu namna ya kufanya matumizi na kuweka akiba. Alisema kuwa kikao hicho kimewahusisha wenyeviti wa serikali za mitaa kwasababu ndio viongozi wa karibu na wananchi. “Hii elimu ya huduma za fedha, tunayowaletea ni mahsusi kwenu kwasababu itawasaidia kufanya maamuzi sahihi wakati wa matumizi. Lakini pia, katika kutunza na kuweka akiba. Huduma ndogo za mikopo ya fedha, mikopo ya vitu na vifaa mbalimbali, mikopo ya nyumba, elimu ya ujasiriamali pamoja na huduma za bima ya afya na bima ya mali ni muhimu kufahamu ili kuwa katika mazingira salama ya ku...

Jiji la Dodoma lapewa angalizo lishe bora kwa wananchi

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Katibu Tawala Mkoa wa Singida, ametembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuelezwa shughuli zinazotolewa katika banda hilo kwa upande wa Divisheni ya Kilimo Mjini. Alielezwa kuwa Kilimo Mjini kinahusiana na kilimo cha kisasa kinachojikita katika mbogamboga na matunda kutokana na ufinyu wa maeneo ya mjini wanapoishi wakulima. Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Athumani Mpanda alieleza kuwa wakulima wanapaswa kutumia maeneo yao madogo waliyonayo kwaajili ya bustani kiroba. “Hizi bustani kiroba tunazitumia kupanda mbogamboga ambazo familia itatumia na hii ni kwasababu kama una kiroba cha kustawisha maua ambayo huyatumii ni vizuri kutumia kuotesha mboga mboga ambazo zitajumuisha lishe na kupendezesha mazingira yetu” alisema Mpanda. Aliongeza kuwa elimu ya bustani za majumbani imeendelea kutolewa katika taasisi nyingi za serikali pamoja na shule za msingi na sekondari. “Tumeanzisha elimu hii kwa lengo la kuhakikisha wakulima na wale ...