Posts

Showing posts from August 1, 2025

RC Dendego apeleka salamu za Waziri Bashe Nanenane

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego aeleza kuwa Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau itaendelea kutekeleza vipaumbele vya kilimo ili kuongeza tija za uzalishaji, kuchangia ongezeko la ajira pamoja na ushiriki wa vijana na wanawake katika sekta ya kilimo. Aliyasema hayo wakati akisoma salamu za Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe wakati wa ufunguzi wa maonesho Nanenane ya wakulima, wafugaji na wavuvi uliofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma kuanzia tarehe 01 – 08 Agosti, 2025. Alisema kuwa zipo hatua zitakazosimamiwa na wizara katika kuhakikisha nchi inakua na chakula cha kutosha wakati wote. “Wizara inatazamia kuimarisha upatikanaji wa chakula na lishe, kuimarisha upatikanaji wa masoko, mitaji na mauzo ya mazao ya kilimo nje ya nchi. Pia kuimarisha maendeleo ya ushirika na kuimarisha matumizi ya mifumo ya TEHAMA katika uendelezaji wa sekta ya kilimo” alisema Dendego. Alimalizia kwa kusema kuwa wizara imeendelea kuwashauri, kuwael...

Dkt. Mpango atoa pongezi maandalizi ya Nanenane

Image
Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango atoa pongezi kwa maboresho katika sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi katika maonesho ya kitaifa ya Nanenane kwa kuongeza matumizi ya teknolojia ya kisasa. Alitoa pongezi hizo wakati wa ufunguzi rasmi wa maonesho ya 32 ya wakulima Nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Dkt. Mpango alieleza kuwa serikali imefanya maboresho makubwa yanayoonekana katika sekta hizo, ikiwemo kuimarisha uhifadhi wa mazao ya wakulima, utoaji wa chanjo kwa mifugo, na utambuzi wa mifugo kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Aidha, alisisitiza dhamira ya serikali kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha chakula barani Afrika kwa kuweka mkazo kwenye uzalishaji wa mazao ya kimkakati yenye thamani kubwa ili kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. “Viongozi wote katika ngazi mbalimbali wanapaswa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sera za kilimo na kuwahimiza w...

Maziwa ya Mama ni kinga kamili kwa Mtoto

Image
  Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wazazi wametakiwa kuhakikisha wanawanyonyesha watoto wao maziwa ya mama kwa kipindi kinachopaswa ili kuwajengea afya bora na kusaidia ukuwaji wa akili zao, hasa katika miaka ya awali. Wito huo ulitolewa na Afisa Lishe wa Jiji la Dodoma, Alfa Fanuel wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Maziwa ya Mama Duniani, yanayofanyika kuanzia tarehe 1-7 Agosti, 2025 uliofanyika katika Kituo cha Afya Ilazo, katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya mwanzo ni msingi muhimu wa afya ya mtoto, na huchangia kwa kiasi kikubwa katika ukuwaji wa ubongo na kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali. “Utafiti unaonesha kuwa watoto wanaonyonyeshwa ipasavyo huwa na uwezo mzuri wa kiakili, kuwa na kinga thabiti ya mwili, huwa na nafasi kubwa ya kuepuka utapiamlo na maradhi ya mara kwa mara” alisema Fanuel. Aidha, alihimiza jamii kuondoa mila na desturi zinazokatisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa...

Kuwahi Kliniki Wajawazito kunaokoa Maisha ya Mama na Mtoto

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wanawake wametakiwa kuhudhulia kliniki pale watakapo gundua kuwa ni mjamzito ili kuhakikisha afya bora ya mama na mtoto tangu hatua za awali za ujauzito na kujua maendeleo ya mtoto na kuepusha magonjwa mbalimbali. Hayo aliyasema Afisa Muuguzi Msaidizi wa Kituo cha Afya Ilazo, Anita Rweyemamu wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji Maziwa ya Mama Duniani, yanayofanyika kuanzia tarehe 1-7 Agosti, 2025. Alisema kuwa wengi wa wanawake wanaanza kuhudhuria kliniki wakiwa tayari na mimba za miezi mitatu au zaidi jambo ambalo ni hatarishi kwa afya ya mama na mtoto. “Niwakumbushe akina mama kuna magonjwa mengi ambayo ni ya kuambukiza na yasio ambukiza yanaweza yakakukumba ikiwa ni ugonjwa wa kifafa cha mimba. Hivyo, basi mama mjamzito anatakiwa aanze kliniki mapema ili aweze kupatiwa huduma muhimu kama chanjo, virutubisho na ushauri wa kiafya. Lakini pia, tunawahimiza wenza wenu kufuatilia na kushiriki kliniki, kwani jukumu la malezi na afya ya mto...

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2025 JIJINI DODOMA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa rai kwa viongozi kutambua wajibu wa kuetekeleza Dira ya Taifa 2050 na mipango ya maendeleo ya sekta ya kilimo ambayo imedhamiria kuongeza kasi ya ukuaji wa kilimo hadi kufikia asilimia 10 kwa mwaka, ifikapo 2030 na kuendelea. Makamu wa Rais ametoa rai hiyo wakati wa ufunguzi wa maonesho na sherehe za wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) zinazofanyika Kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma. Amesema viongozi ni vema kuwajibika kuwaelekeza wakulima, wafugaji na wavuvi kuweka nguvu zaidi kwenye mazao yenye thamani kubwa sokoni, kuwekeza katika uzalishaji wa kisasa ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje, kuvutia wawekezaji wa ndani na nje pamoja na kuwekeza katika miundombinu baridi ya uhifadhi na usafirishaji. Ameongeza kwamba ni vema Viongozi kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika teknolojia za kisasa za kilimo, ikiwemo kilimo-janja, uwekezaji katika umwagiliaji, upatikanaji wa fedha na m...

DC Shekimweri awakaribisha wananchi kushiriki maonesho ya Nanenane

Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya maboresho ya miundombinu katika viwanja vya maonesho ya Siku ya Wakulima Duniani. Hayo aliyasema wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kuwakaribisha wananchi wote wa Jiji la Dododma na vionga vyake katika maonesho ya Siku ya Wakulima Duniani yanayohusu tasnia ya uvuvi, kilimo na mifugo yatakayofanyika katika viwanja vya Nanenane vilivyopo Kata ya Nzuguni, jijini Dodoma. Alisema kuwa kwa maonesho ya wakulima duniani kwa mwaka 2025 katika Jiji la Dodoma yamekuwa na mabadiliko ya hali ya juu. “Kupitia maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alitaka mahema yajengwe ya kisasa na ya kudumu. Hivyo, maagizo hayo tumetekeza kwa kiasi kikubwa. Pia kwa upande wa barabara tumeweka miundombinu mizuri ya barabara ili kuepusha vumbi. Hivyo, kwa wale watakaokuja katik...

DC Dodoma awapongeza wahitimu mafunzo ya stakabadhi

Na. Veronica Elias, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amewapongeza wakufunzi wa semina ya usimamizi wa mafunzo ya stakabadhi kutoka wizarani na washiriki waliohitimu mafunzo hayo na kusema kuwa ni mafunzo muhimu. Akizungumza na waandishi wa habari Shekimweri alisema kuwa mafunzo hayo yanaumuhimu kwa wakulima na wafanyabiashara kwasababu yanawawezesha kuona faida ya kile wanachokifanya pamoja na kupata mabalozi wengine kwaajili ya kwenda kutoa elimu kwa wakulima. Alisema kuwa kutakuwa na mfumo rasmi wa kuratibu tasnia ya mazao mchanganyiko ilikusudi mkulima alindwe na anufaike na jasho lake kupitia nguvu na gharama alizopoteza kwenye uwekezaji huo Pamoja na wafanyabiashara kupata haki yao ya msingi kutokana na matarajio yao waliokusudia. “Najisikia furaha sana kufika katika semina hii kwasababu moja ya maoni yangu binafsi, mfumo wa stakabadhi wakati fulani unakutana na wapinzani kwa sababu ni kitu kipya ambacho hawakijui kwa muda huo. Hivyo, asilimia kubwa ya watu k...

Wananchi wahamasishwa kujitokeza kuapata huduma Kanda ya Viwandani, Dodoma

Image
Na. Veronica John, DODOMA   Mkuu wa Kanda ya utoaji huduma ya Viwandani katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lucas Nkelege amewataka maafisa waliopangwa katika kanda hiyo kuhamasisha wananchi wote wanaojitokeza kupata huduma wanapatiwa huduma kwa viwango vya juu ili waweze kujivunia utendaji kazi wa wafanyakazi hao wa serikali. Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akiongea na wafanyakazi waliopangwa katika kanda hiyo na viongozi wa serikali za mitaa katika kuitambulisha kanda ya utoaji huduma ya Viwandani iliyopo katika jengo la Soko la wazi la Machinga, eneo la Bahi road jijini Dodoma. Alisema kuwa moja ya jambo muhimu ni kuhakikisha wananchi wa kata zote wanapata huduma kwa urahisi. “Katika kanda hii ya Viwandani, tuna kata saba ambazo tutazihudumia. Hivyo, nitumie nafasi hii kuwasisitiza tu utoaji huduma bora na za viwango ili wananchi wafurahie utumishi wetu. Huduma zote zitatolewa hapa, ila nisisitize zaidi eneo la utoaji wa leseni za biashara na ushuru wa huduma. Nimeamua kutaj...