Shule mpya ya Msingi Chinyoyo ya kwanza kujengwa Kata ya Kilimani
Na. Emmanuel Charles, KILIMANI Mradi wa ujenzi wa shule mpya ya Chinyoyo, Kata ya Kilimani unaogharimu shilingi 147,000,000 ni shule ya kwanza kujengwa katani hapo na itaondoa adha ya wanafunzi ya kutembea umbali mrefu kufuata masomo. Haya yalisemwa na Diwani wa Kata ya Kilimani, Neema Mwaluko wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ‘Media Tour’ kukagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali kuanzia 2021-2025 katika kata hiyo. Alisema kuwa kwasababu kata yake ipo mjini, miundombinu ikiwemo ya elimu ilichelewa kufika na sasa serikali ya awamu ya sita inajenga shule ya msingi ili kuwakwamua watoto wanaotembea umbali mrefu. “Kwa miaka yote ya nyuma, kata hii haikuwahi kuwa na shule yeyote na wanafunzi wanalazimika kutembea umbali mrefu kufuata masomo katika kata za jirani. Tunaishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutuona na kuamua kutenga eneo la kujenga Shule ya Msingi Chinyoyo kwa gharama ya shilingi 147,000,000 ambapo ujenzi wa madarasa manne na ofisi mbili...